SURA YA 114
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI
[SUBSIDIARY LEGISLATION]
INDEX TO SUBSIDIARY LEGISLATION
ORODHA YA KANUNI
Kanuni
Jina
SEHEMU YA I
MAMBO YA AWALI
1. Jina.
2. Ufafanuzi.
SEHEMU YA II
USIMAMIZI NA UTAWALA
3. Taarifa.
4. Amri.
5. Wito.
6. Viapo.
7. Utaratibu wakati taasisi za kijiji zinasikiliza mashauri.
SEHEMU YA III
FIDIA
8. Nani aweza kudai fidia.
9. Misingi ya ukadiriaji.
10. Bei katika soko.
11. Mthamini aliyehitimu.
12. Mthamini Mkuu.
13. Fidia.
14. Posho ya upangaji.
15. Kupoteza faida.
16. Posho ya usumbufu.
17. Posho ya usafiri.
18. Ardhi isiyokaliwa.
19. Riba.
20. Kupewa taarifa ya kudai fidia.
21. Madai ya fidia.
22. Msaada wa kutayarisha madai ya fidia.
23. Kukubali madai ya fidia.
24. Usuluhishi kuhusu madai ya fidia.
25. Aina za fidia.
SEHEMU YA IV
USIMAMIZI WA PAMOJA WA ARDHI YA KIJIJI
26. Pendekezo la usimamizi wa pamoja wa ardhi ya kijiji.
27. Kupigia kura pendekezo la usimamizi wa pamoja wa ardhi ya kijiji.
28. Kukataliwa kwa pendekezo la usimamizi wa pamoja wa ardhi ya kijiji.
29. Uteuzi wa Kamati ya Pamoja.
30. Tafakari ya rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja.
31. Marekebisho ya rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja.
32. Makubaliano ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja.
33. Kamati ya Pamoja inawajibika kwa uendeshaji wa usimamizi wa pamoja.
34. Vipengele vinavyoelekeza uendeshaji wa Kamati ya Pamoja.
35. Yaliyomo katika Mpango wa Usimamizi wa Pamoja.
SEHEMU YA V
DAFTARI LA ARDHI YA KIJIJI
36. Sehemu za Daftari.
37. Cheti cha Ardhi ya Kijiji.
38. Daftari la Hati.
39. Daftari Bayana la Kutahadharisha.
40. Watu wanaostahili kuwasilisha nyaraka kwa ajili ya usajili.
41. Taratibu za usajili.
42. Utoaji wa namba na hifadhi ya nyaraka zilizosajiliwa.
43. Kumbukumbu kimaandishi iliyoambatishwa na waraka uliosajiliwa.
44. Kitabu cha muhtasari.
45. Shughuli za miliki za ardhi.
46. Mwenye haki kutaarifiwa.
47. Jukumu la Afisa kwenye shughuli za ardhi.
48. Kipaumbele.
49. Afisa aweza kukataa kusajili nyaraka.
50. Uwezo wa Afisa kusahihisha makosa.
51. Usajili hautaondoa kasoro au kuhalalisha.
52. Daftari laweza kukaguliwa na nakala kupatikana.
53. Nyaraka mbadala ya iliyosajiliwa.
54. Nakala ya waraka uliyosajiliwa.
55. Kupatikana waraka asili uliyosajiliwa.
56. Kupatikana nakala ya waraka uliosajiliwa.
57. Nakala ya waraka potevu uliyosajiliwa.
58. Nakala iliyothibitishwa ya waraka uliyosajiliwa kukubalika katika kesi za madai.
59. Matumizi ya nakala iliyothibitishwa ya waraka uliyosajiliwa katika kesi za madai.
60. Muda wa Masjala kuwa wazi.
SEHEMU YA VI
UAMUZI WA MASLAHI NA MIPAKA KATIKA ARDHI
61. Taarifa kwa pande zinazohusika.
62. Kuweka mipaka.
63. Uthibitisho wa mipaka.
64. Kusafisha na kuweka alama kwenye mipaka.
65. Kutunza mipaka.
66. Kipimo cha upimaji.
67. Matayarisho ya mchoro.
68. Taratibu za upimaji.
69. Kuweka kumbukumbu ya haki za njia.
70. Mgao wa mchoro.
71. Kumbukumbu za uamuzi wa maslahi na mipaka katika ardhi.
72. Taarifa ya upimaji wa ardhi inayomilikiwa kwa hakimiliki ya kimila iliyosajiliwa.
73. Namba ya Utambulisho wa Kipande cha Ardhi.
74. Mgawanyo.
SEHEMU YA VII
MENGINEYO
75. Waziri aweza kuweka viwango vya juu vya kumiliki ardhi.
76. Taratibu za idhini ya viwango vya juu vya kumiliki ardhi.
77. Misingi ya jumla ya usuluhishi.
78. Maandalizi ya nyaraka.
79. Fomu zitakazotumika kuhusiana na Sheria na Kanuni hizi.
80. Mabadiliko ya fomu.
81. Ada.
82. Faini.
83. Ushuhuda wa Kusaini Nyaraka.
JEDWALI LA KWANZA
FOMU
SEHEMU YA I
USIMAMIZI NA UTAWALA
Fomu Na. 1 Amri ya kuitwa kwenye Kamati ya Uamuzi ya Kijiji.
Fomu Na. 2 Amri ya kuwasilisha nyaraka mbele ya Kamati ya Uamuzi ya Kijiji.
Fomu Na. 3 Wito wa kuhudhuria kusikilizwa mbele ya Kamati ya Uamuzi wa Kijiji.
Fomu Na. 4 Wito wa kuhudhuria kusikilizwa mbele ya Baraza la Ardhi la Kijiji.
Fomu Na. 5 Kiapo cha shahidi.
Fomu Na. 6 Taarifa ya kusudio la kutangaza ardhi yenye madhara.
Fomu Na. 7 Taarifa ya kuitangaza ardhi yenye madhara.
Fomu Na. 8 Taarifa ya kusudio la kuhawilisha Ardhi ya Kijiji kuwa ardhi ya kawaida au ardhi ya hifadhi.
Fomu Na. 9 Taarifa ya kuhawilisha Ardhi ya kijiji.
Fomu Na. 10 Tamko la mgongano wa maslahi.
SEHEMU YA II
FIDIA
Fomu Na. 11 Taarifa kwa Halmashauri ya Kijiji kudai fidia.
Fomu Na. 12 Ombi la Halmashauri ya Kijiji kulipwa fidia.
Fomu Na. 13 Kibali cha fidia.
Fomu Na. 14 Taarifa kwa mkazi kudai fidia.
Fomu Na. 15 Ombi la mkazi kudai fidia.
SEHEMU YA III
DAFTARI LA ARDHI YA KIJIJI
Fomu Na. 16 Cheti cha Ardhi ya Kijiji.
Fomu Na. 17 Kitabu cha Muhtasari.
SEHEMU YA IV
HAKIMILIKI ZA KIMILA
Fomu Na. 18 Ombi la hakimiliki ya Kimila.
Fomu Na. 19 Ahadi ya toleo la hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 20 Kukubali ahadi ya Toleo la Hakimiliki ya Kimila.
Fomu Na. 21 Cheti cha Hakimiliki ya Kimila.
Fomu Na. 22 Ombi la nakala ya Cheti cha Hakimiliki ya Kimila.
Fomu Na. 23 Taarifa ya kulipa kodi.
Fomu Na. 24 Taarifa ya Uhakilishaji wa Hakimiliki ya Kimila.
Fomu Na. 25 Kukubaliwa Kukataliwa kwa uhakilishaji wa hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 26 Ombi la kibali cha kutoa hakimiliki isiyo asili.
Fomu Na. 27 Cheti cha kibali cha hakimiliki isiyo asili upangishaji leseni haki ya matumizi.
Fomu Na. 28 Ombi la kutoa hakimiliki isiyo asili kwenye kijiji.
Fomu Na. 29 Kutolewa kwa hakimiliki isiyo isili kwenye ardhi ya kijiji.
Fomu Na. 30 Kurejesha hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 31 Barua ya onyo.
Fomu Na. 32 Kibali kwa hatua ya Halmashauri ya Kijiji.
Fomu Na. 33 Ilani ya kujieleza.
Fomu Na. 34 Taarifa ya kulipa taini.
Fomu Na. 35 Taarifa ya kurekebisha ukiukaji wa masharti.
Fomu Na. 36 Amri ya Usimamizi.
Fomu Na. 37 Ombi la idhini ya uhakilishaji kwa muda.
Fomu Na. 38 Taarifa ya uhakilishaji kwa muda wa hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 39 Agizo la masharti ya uhakilishaji kwa muda.
Fomu Na. 40 Leseni ya Makazi.
Fomu Na. 41 Taarifa ya kubaini utelekezaji ardhi.
Fomu Na. 42 Tamko la utelekezaji ardhi.
SEHEMU YA V
UAMUZI KUHUSU MASLAHI NA MIPAKA KATIKA ARDHI
Fomu Na. 43 Ombi la kibali kuhusu shughuli ya ardhi mavozidi kiwango cha juu cha ardhi kwa kijiji.
Fomu Na. 44 Ombi la Maamuzi kwa Eneo Maalumu.
Fomu Na. 45 Pendekezo la kutumia Uamuzi Ngazi ya Kijiji.
Fomu Na. 46 Taarifa ya Kamati ya Uamuzi ya Kijiji kusikiliza masuala ya ardhi.
Fomu Na. 47 Uthibitisho wa mipaka.
Fomu Na. 48 Taarifa ya upimaji wa mipaka ya hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 49 Kugawanya hakimiliki ya kimila.
Fomu Na. 50 Kumbukumbu ya uamuzi wa maslahi na mipaka ya ardhi.
JEDWALI LA PILI
ADA
JEDWALI LA TATU
FAINI
KANUNI ZA ARDHI YA VIJIJI
(Zimetungwa chini ya fungu la 65)
G.N. No. 201 of 2002
SEHEMU YA I
MAMBO YA AWALI
1. Jina
Kanuni hizi ziitwe Kanuni za Ardhi ya Vijiji, 2002.
2. Ufafanuzi
Katika Kanuni hizi, isipokuwa tu pale ambapo maelezo yanahitaji vinginevyo:–
"Afisa" maana yake ni Afisa Mtendaji wa kijiji;
"Afisa Ardhi wa Wilaya" maana yake ni Afisa Mteule aliyeteuliwa chini ya kifungu cha 11 cha Sheria ya Ardhi;
"Afisa Mtendaji wa Kijiji" maana yake ni mtu aliyeteuliwa kuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji kwa mujibu wa sheria husika;
"Baraza" maana yake ni Baraza la Ardhi la Kijiji lililoundwa chini ya fungu la 60 la Sheria;
"Daftari la Ardhi ya Kijiji" maana yake ni daftari la ardhi ya kijiji linalotunzwa kwa mujibu wa fungu la 21 la Sheria;
"daimiliki kwa nyaraka zilizowasilishwa" maana yake ni kuwasilisha waraka wowote uliotajwa katika aya za (ii), (iv) na (v) za ibara ya (b) ya kifungu cha (6) cha fungu la 112 la Sheria ya Ardhi;
"hakimiliki isiyo asili" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa na Sheria;
"hakimiliki ya kimila" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa na Sheria;
"Kamati" maana yake ni Kamati ya Uamuzi ya Kijiji iliyoundwa chini ya fungu la 53 la Sheria, na ni pamoja na Afisa Mwamuzi anayetumia mamlaka yake chini ya Fungu la 56 la Sheria;
"Mahakama" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa na Sheria;
"Mamlaka ya Serikali ya Mtaa" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa katika fungu la 2 la Sheria;
"Masjala ya Ardhi ya Wilaya" maana yake ni Masjala ya Ardhi ya Wilaya iliyoanzishwa chini ya Sheria ya Usajili;
"maslahi katika shauri" maana yake ni maslahi, kifedha au vinginevyo, yanayoweza kupunguza ubora wa wajibu wa mtu katika kusikiliza na kuamua jambo lolote, na ni pamoja na maslahi ya ndugu wa damu au kutokana na uhusiano wa ndoa;
"mkazi" maana yake ni mmiliki wa hakimiliki ya kimila;
"Mthamini Aliyehitimu" maana yake ni kama ilivyofafanuliwa kwenye fungu la 2 la Sheria ya Ardhi *;
"rehani isiyo rasmi" maana yake ni rehani kama ilivyofafanuliwa kwenye ibara (a) ya kifungu cha (6) cha fungu la 112 la Sheria ya Ardhi;
"Serikali" maana yake ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
"Sheria" maana yake ni Sheria ya Ardhi ya Vijiji *;
"taasisi ya kijiji" maana yake ni Halmashauri ya Kijiji, Kamati ya Halmashauri ya Kijiji, Kamati ya uamuzi Ngazi ya Kijiji na Afisa Mwamuzi anayetekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa fungu la 56 la Sheria.
"utaratibu wa usimamizi wa pamoja" maana yake ni utaratibu wa usimamizi wa ardhi ya kijiji unaoweza kuwekwa kwa mujibu wa fungu la 8 la Sheria;
"waraka uliosajiliwa" maana yake ni cheti cha hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo asili kinachotolewa kwa mujibu wa sehemu ya IV ya Sheria, kilichomo kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi,
SEHEMU YA II
USIMAMIZI WA UTAWALA
3. Taarifa
Taarifa ya kusikilizwa kwa shauri lolote na taasisi ya kijiji kwa mujibu wa Kanuni hizi itatolewa kama ilivyo kwenye Jedwali la Kwanza.
4. Amri
Amri mayomtaka mtu ahudhurie kikao au awasilishe waraka mbele ya taasisi ya kijiji itaandikwa kwenye fomu maalum zilizoonyeshwa katika Jedwali la Kwanza.
5. Wito
(1) Wito unaotolewa na Mwenyekiti wa Kamati, au Afisa Mwamuzi anayetumia mamlaka chini ya fungu la 56 la Sheria, kwa mtu anayetakiwa kuhudhuria kwa mujibu wa fungu la 54 la Sheria ya Ardhi ya Vijiji lazima umpe taarifa ya siku zisizopungua 14 kabla ya tarehe anapotakiwa kuhudhuria kusikilizwa shauri.
(2) Wito kwa mujibu wa kanuni hii utatolewa kama ulivyoonyeshwa kwenye Jedwali la Kwanza.
6. Viapo
Kiapo anachoweza kuapisha Mwenyekiti wa Kamati au Afisa Mwamuzi anayetumia mamlaka chini ya fungu la 56 la Sheria kinaweza kuwa kama kilivyoonyeshwa kwenye Jedwali la Kwanza.
7. Utaratibu wakati taasisi za kijiji zinasikiliza mashauri
Katika kusikiliza mashauri kwa mujibu wa Sheria au Kanuni Hizi, taasisi ya kijiji itawajibika kufuata taratibu za msingi ya haki za binadamu katika kuweka taratibu zake, na itawajibika–
(a) kuendesha usikilizaji wa mashauri hadharani na bila ya urasimu lakini kwa kufuata utaratibu, heshima na usawa kwa pande zote kufafanua wazi kwa wawakilishi wowote na taasisi hiyo ya kijiji itazingatia zaidi maswala ya msingi katika shauri lililoletwa na itatoa uamuzi juu ya haki bila kulazimika kuzingatia taratibu za kiufundi;
(b) kutomshirikisha katika kikao mjumbe wa taasisi ya kijiji mwenye maslahi katika shauri linalojadihwa, maslahi ambayo mjumbe huyo atawajibika kuyatangaza na kutohudhuria kikao wala kujihusisha kwa namna yoyote ile katika kusikiliza kama mjumbe wa taasisi ya kijiji;
(c) kabla ya kusikiliza shauri, kupanga na kutangaza saa ya mchana ya siku ambapo shauri litasikilizwa na katika kufanya hivyo itazingatia mazingira ya pande husika na mpangilio wa kawaida wa kazi katika eneo ambako shauri litasikilizwa;
(d) kuruhusu watu wote wanaotaka kutoa hoja mbele ya taasisi ya kijiji wafike mbele ya taasisi hiyo wao binafsi au kwa kuwakilishwa;
(e) kuruhusu mtu aliyeitwa shaurini atoe hoja yake kwanza na ndipo ahojiwe kuhusu jambo lolote kutokana na hoja yake, au aombwe na mjumbe aliyepo au mtu mwenye maslahi katika ardhi inayohusika katika shauri, kutoa taarifa za ziada kuhusu hoja yake;
(f) baada ya mtu aliyeitwa kutoa hoja yake, kuruhusu mtu yeyote aliye na madai juu ya ardhi husika atoe hoja yake na kuulizwa maswali na mjumbe yeyote aliyepo wa taasisi ya kijiji, na mtu yeyote aliyeitwa shaurini;
(g) Kuhusu mtu yeyote alete maelezo kwa mdomo au kimaandishi au kwa mdomo na pia kimaandishi;
(h) endapo taasisi ya kijiji itakusudia kuitisha ushahidi juu ya jambo au suala lolote, itawataarifu wahusika wa pande zote za shauri kuhusu uamuzi huo na kuwaruhusu kutoa maoni au kuuliza maswali kuhusu ushahidi huo;
(i) endapo taasisi ya kijiji itatembelea na kukagua ardhi mayohusika katika shauri linalosikilizwa, itaruhusu watu wanaodai kuwa na maslahi katika ardhi hiyo, waonyeshe alama za ardhi hiyo na watoe maelezo mengine kuhusu ardhi hiyo na maslahi yao katika ardhi hiyo;
(j) kwa kumtumia Mwenyekiti wa taasisi ya kijiji, au mjumbe, au afisa aliyeteuliwa na Mwenyekiti kwa ajili hiyo, kutunza kumbukumbu ya uendeshaji wa shauri lililosikilizwa, pamoja na kumbukumbu ya kutembelea ardhi yoyote wakati wa kusikiliza shauri;
(k) yaweza kukubali kama ushahidi kuhusu mipaka ya eneo la ardhi mayohusika katika shauri:
(i) tamko kuhusu mipaka litolewalo na mtu yeyote anayetambuliwa na jamii kama mtu mwaminifu na anayefahamu masuala ya ardhi katika kijiji;
(ii) aina rahisi au za kiasili za upimaji au uwekaji mipaka kwa kutumia alama asili na miti au majengo na vitu vinginevyo vinavyoonekana dhahiri;
(iii) shughuli za binadamu kwenye ardhi kama vile matumizi ya njia za miguu, mapito ya mifugo sehemu za kupata maji na uwekaji alama za mipaka katika ardhi;
(iv) ramani na michoro iliyochorwa kwa vipimo au bila vipimo rasmi mayoonyesha kwa rejea, jambo lolote lililotajwa katika aya ya (ii) au ya (iii) za ibara (K) mipaka ya eneo la ardhi;
(l) kuzingatia kwa umakini wa kipekee maslahi katika ardhi mayohusika na kusikiliza shauri linalowahusu wanawake, watoto na watu wasiojiweza, na kuhakikisha kwamba maslahi haya yanazingatiwa na kuwekewa kumbukumbu kikamilifu;
(m) katika kuamua kama mafaa kuahirisha usikilizaji wa shauri, yaweza kuahirisha shauri kwa lengo la kuzirahisishia pande husika kuondoa wao wenyewe tofauti walizonazo kuhusu maslahi ya kila upande katika ardhi na lazima kunukuu mapatano yoyote waliyoyafanya shauri litakapoanza tena kusikilizwa;
(n) kuzingatia uwezekano wakati wowote au baada ya kusikiliza jambo fulani, kutoa uamuzi wa awali kuhusu suala lolote, endapo itafanya uamuzi wa aina hii, iwaombe pande zote kutoa maoni yao juu ya uamuzi huo kwa mdomo au kwa maandishi;
(o) kujaribu kufikia maamuzi yote kwa muafaka lakini kama haitawekana, basi uamuzi wa walio wengi waweza kuchukuliwa na zinukuliwe sababu za uamuzi wa wengi na za wale wachache;
(p) katika kufikia uamuzi kama suala lolote limethibitishwa mbele ya taasisi ya kijiji, kuamua kama kumetolewa ushahidi wa kutosha yaani kama, uzito wa, hoja unaashiria zaidi kwamba jambo limethibitishwa kuliko kutothibitishwa;
(q) kuandaa taarifa itakayojumuisha–
(i) majina ya wajumbe wa taasisi ya kijiji iliyosikiliza shauri;
(ii) tarehe ya kusikiliza shauri;
(iii) majina ya watu wa pande husika;
(iv) muhtasari wa ushahidi wa pande zote na vya mashahidi wote;
(v) maamuzi kuhusu vipengele vyote vya shauri na madai pamoja na sababu za mapendekezo hayo;
(vi) mapendekezo kwa vipengele vyote wa shauri na madai pamoja na sababu za mapendekezo hayo;
(r) kusaini ripoti iliyotayarishwa kwa mujibu wa ibara (q).
SEHEMU YA III
FIDIA
8. Nani aweza kudai fidia
Wafuatao waweza kudai fidia kutokana na uhawilishaji wa ardhi ya kijiji kuwa ardhi ya kawaida au ardhi ya hifadhi chini ya fungu la 4 la Sheria, au kutokana na ardhi kutangazwa kuwa ardhi yenye madhara chini ya fungu la 6 la Sheria, na endapo Halmashauri ya Kijiji imeamua kwamba wakazi watatakiwa kuihama ardhi hiyo yenye madhara au sehemu ya ardhi hiyo:
(a) Halmashauri ya Kijiji kwa niaba ya wanakijiji waliopoteza ardhi ya pamoja ya kijiji, mali na mafao kutokana na ardhi ya pamoja ya kijiji;
(b) Mwanakijiji yeyote anayekalia ardhi iliyohawilishwa au ardhi yenye madhara chini ya hakimiliki ya kimila, bila kujali kama hakimiliki hiyo imesajiliwa au la.
9. Misingi ya ukadiriaji
Msingi wa kukadiria thamani ya ardhi yoyote na uboreshaji usiohamishika kwa ajili ya ulipaji wa fidia chini ya Sheria ni thamani ya ardhi hiyo katika soko.
10. Bei katika soko
Thamani ya ardhi katika soko inayoihusu ardhi yoyote na uboreshaji usiohamishika kutumia kigezo cha mlinganisho wa mauzo hali halisi ya karibuni ya ardhi au mali kama hiyo au kwa kutumia kigezo cha mapato au gharama ya kufidia endapo ardhi au mali ni ya aina yake ambayo haiwezi kuuzwa.
11. Mthamini aliyehitimu
Kila makadirio ya thamani ya ardhi na ya uboreshaji usiohamishika kwa malengo ya Sheria hii lazima yafanywe na mthamini aliyehitimu.
12. Mthamini Mkuu
Kila makadirio ya thamani ya ardhi na uboreshaji usiohamishika kwa ajili ya kulipa fidia itakayolipwa na Serikali Kuu au Serikali za Mitaa lazima yathibitishwe na Mthamini Mkuu wa Serikali au mwakilishi wake.
13. Fidia
Fidia kwa kupoteza maslahi yoyote kwenye ardhi itajumuisha thamani ya uboreshaji usiohamishika, posho ya usumbufu, posho ya usafiri, posho ya upangaji na kupoteza faida.
14. Posho ua upangaji
Kodi ya pango katika soko kwa jengo itakadiriwa na kuzidishwa mara miezi thelathini na sita (36) ili kupata posho ya upangaji itakayolipwa.
15. Kupoteza faida
Faida halisi kwa mwezi kwa biashara inayoendeshwa kwenye ardhi itakadiriwa na kuzidishwa mara miezi thelathini na sita (36) ili kufikia kiwango cha malipo ya faida inayopotea.
16. Posho ya usumbufu
Posho ya usumbufu itakadiriwa kwa kuzidisha thamani ya ardhi mara wastani wa asilimia ya riba inayotolewa na Benki za Kibiashara kwa akiba ya muda maalum ya miezi kumi na miwili (12) wakati wa kupoteza ardhi.
17. Posho ya usafiri
Posho ya usafiri itakuwa gharama halisi ya kusafirisha tani kumi na mbili (12) za mizigo kwa reli au barabara (kutegemea njia ya gharama nafuu) hadi umbali usiozidi kilomita ishirini (20) kutoka mahali pa kuondoshwa.
18. Ardhi isiyokaliwa
Posho za usafiri, upangaji na kupoteza faida hazitalipwa kwa ardhi isiyokaliwa wakati maslahi katika ardhi yanapotezwa.
19. Riba
(1) Riba za usafiri, upangaji na kupoteza faida Kuu au Mamlaka ya Serikali ya Mtaa pale tu ambapo malipo ya fidia hayakulipwa kwa wakati.
(2) Kwa ajili ya ukadiriaji wa riba kwenye fidia mayotakiwa "kulipwa kwa wakati" maana yake ni kulipa fidia katika kipindi cha miezi sita baada ya ardhi mayohusika kutwaliwa au hakimiliki kubatilishwa.
(3) Endapo kiwango cha fidia hakilipwi miezi sita (6) baada ya ardhi kutwaliwa au hatimiliki kubatilishwa riba italipwa kwa wastani wa asilimia ya riba mayolipwa na Benki za kibiashara kwenye akiba za muda maalum hadi fidia itakapolipwa.
20. Kupewa taarifa ya kudai fidia
Pale ambapo fungu la 4 na la 6 yanahusika, Kamishna atatoa taarifa, kwa fomu iliyoko katika Jedwali la Kwanza, kwa Halmashauri ya Kijiji na watu wote wanaokalia ardhi kwa hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo asili kwenye eneo la ardhi linalohusika na taarifa ya kuhawilisha ardhi ya kijiji au, kwa kadiri itakavyokuwa, taarifa ya kutangaza ardhi yenye madhara katika Halmashauri ya Kijiji na watu wote waliotajwa katika kanuni hii walete madai yao ya fidia.
21. Madai ya fidia
Madai ya fidia yatawasilishwa kwa fomu iliyopo katika Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi katika kipindi kisichopungua siku sitini baada ya kupokelewa taarifa iliyotajwa katika kanuni ya 20.
22. Msaada wa kutayarisha madai ya fidia
Afisa Mteule, kutokana na ombi la Afisa wa Kijiji ambacho ardhi yake imetolewa taarifa chini ya fungu la 4 la Sheria kuhusu kuhawilisha ardhi ya kijiji, au taarifa chini ya fungu la 6 la Sheria kuhusu kutangaza ardhi ya kijiji kuwa ardhi yenye madhara atalazimika kusaidia kijyi hicho na watu wanaokalia maeneo ambayo yametolewa matangazo namna ya kuandaa na kuwasilisha madai ya fidia.
23. Kukubali madai ya fidia
(1) Kamishna, katika kipmdi kisichozidi siku tisini kutoka tarehe madai yalipowasilishwa, ataamua ama ayakubali au ayakatae maombi hayo au sehemu yake.
(2) Endapo Kamishna atakubali madai yoyote ya fidia yaliyowasilishwa chini ya kanuni ya 21, basi atatoa taarifa kwa Waziri.
(3) Katika kipindi kisichopungua siku ishirini na moja tangu Waziri kupokea taarifa, Kamishna atafanya utaratibu wa kumwezesha mdai alipwe fidia.
24. Usuluhishi kuhusu madai ya fidia
(1) Endapo Kamishna ataamua kutokubali madai ya fidia iwapo mdai na Kamishna wataafikiana, madai hayo yanaweza kurejeshwa kwa mtu atakayeteuliwa na Waziri kuwa msuluhishi wa suala hilo.
(2) Endapo msuluhishi atafaulu kupatanisha pande husika, atampeleka Waziri taarifa ya upatanisho huo, na Kamishna katika kipindi cha siku ishirini na moja tangu Waziri apokee taarifa kutoka kwa msuluhishi, atafanya utaratibu wa kumwezesha mdai alipwe fidia.
(3) Endapo msuluhishi, baada ya siku zisizopungua tisini za majadiliano kati ya pande husika, atashindwa kuzisaidia kufikia makubaliano katika suala la madai ya fidia au endapo pande zote husika au upande mmoja wapo hautaki kupeleka suala la madai kwa msuluhishi, basi suala hilo litapelekwa kwenye Mahakama yenye mamlaka.
25. Aina za Fidia
(1) Fidia kwa mujibu wa fungu la 4 na la 6 la Sheria na Kanuni ya 13 yaweza kutolewa kwa namna au mojawapo ya namna zifuatazo:–
(a) ardhi inayofanana kwa ubora, ukubwa na uwezo wa kuzalisha kama ardhi iliyopotea;
(b) jengo linalofanana kwa ubora, ukubwa na matumizi kama jengo lililopotea;
(c) mimea na miche;
(d) fursa ya kutumia mali za jumuiya;
(e) kiasi cha fedha sawa na thamani ya uboreshaji usiohamishika wa ardhi iliyohawilishwa au ardhi iliyotangazwa kuwa ardhi yenye madhara, au malipo ya fidia kwa kupunguza eneo la ardhi ama kwa upotevu au uharibifu wa ardhi ambayo inaweza kutumika kuzalisha, au malipo kwa ajili ya usumbufu uliosababishwa na uhawilishaji wa ardhi au ardhi kutangazwa kuwa ardhi yenye madhara;
(f) kupewa mara kwa mara nafaka na vyakula vingine mbalimbali kwa kipindi kitakachowekwa;
(g) namna nyingine za fidia zinazoweza kukubalika kati ya mdai na Kamishna.
SEHEMU YA IV
USIMAMIZI WA PAMOJA WA ARDHI YA KIJIJI
26. Pendekezo la Usimamizi wa pamoja wa Ardhi ya Kijiji
Pendekezo la usimamizi wa pamoja wa ardhi ya kijiji baina ya vijiji viwili, au kijiji na Halmashauri ya Wilaya au mamlaka ya mji, laweza kutolewa na Kamishna wa Ardhi kwa Halmashauri za Vijiji na Halmashauri za Wilaya au Halmashauri ya Mji, au laweza kutolewa na halmashauri ya kijiji kwa halmashauri ya kijiji kingine au mamlaka yoyote ya mtaa, au laweza kutolewa kwa halmashauri ya kijiji ambacho inapendekezwa kuundwa kwa usimamizi huo wa pamoja nayo.
27. Kupigia kura pendekezo la Usimamizi wa Pamoja wa Ardhi ya Kijiji
Pendekezo lililotajwa katika Kanuni ya 2 lazima lifikiriwe na lipigiwe kura na halmashauri za vijiji na halmashauri za mamlaka za mitaa zinazohusika.
28. Kukataliwa kwa pendekezo la Usimamizi wa Pamoja wa Ardhi ya Kijiji
Endapo pendekezo litakataliwa na halmashauri ya kijiji au mamlaka ya mtaa, lazima kipindi kisichopungua miezi mitatu kipite ndipo pendekezo hilo au pendekezo lenye marekebisho laweza kuletwa lifikiriwe tena na halmashauri ya kijiji au halmashauri ya mamlaka ya mtaa iliyokataa pendekezo la awali.
29. Uteuzi wa Kamati ya pamoja
Halmashauri za vijiji na mamlaka za mitaa zinazopiga kura kukubali uundaji wa mpango wa usimamizi wa pamoja, kila moja itateua watu wasiopungua watatu na wasiozidi watano kuwa wajumbe wa Kamati ya Pamoja ili waandae Mpango wa Usimamizi wa Pamoja.
30. Tafakari ya Rasimu ya Mpango wa Usimamizi pamoja
Baada ya Kamati ya Pamoja kuafikiana kuhusu rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja, itapeleka rasimu hiyo katika mkutano wa kijiji na halmashauri ya mamlaka ya mtaa husika kwa ajili ya vyombo hivyo kuufikiria na kuupigia kura mpango huo.
31. Marekebisho ya Rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja
Mkutano wa kijiji na halmashauri ya mamlaka ya mtaa vinaweza kupendekeza marekebisho katika rasimu ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja, na mapendekezo yoyote ya marekebisho yatawasilishwa kwa Kamati ya pamoja ili yafikiriwe.
32. Makubaliano ya Mpango wa Usimamizi wa Pamoja
Mpango wa Usimamizi wa pamoja hautatekeleza hadi hapo kila kijiji na kila mamlaka ya mtaa husika katika mpango huo waafiki vipengele vya mpango huo na wawe wamepiga kura ya kuupokea mpango huo.
33. Kamati ya Pamoja inawajibuka kwa uendeshaji wa usimamizi wa Pamoja
Kamati ya Pamoja iliyoundwa kuandaa Mpango wa Usimamizi wa Pamoja itakuwa na jukumu la utekelezaji wa Makubaliano ya Matumizi ya Pamoja ya Ardhi na itakutana si chini ya mara moja kila miezi mitatu kuhakikisha kunakuwepo uendeshaji madhubuti na rahisi.
34. Vipengele vinavyoelekeza uendeshaji wa Kamati ya pamoja
Kamati ya Pamoja iliyoundwa chini ya Kanuni hizi itaongozwa na kufuata miongozi inayoongoza shughuli za kamati zilizowekwa chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya).
35. Yaliyomo katika mpango wa usimamizi wa Pamoja
Mpango wa Usimamizi wa Pamoja utashughulikia usimamizi wa ardhi ya kijiji kinachohusika na bila ya kuathiri ujumla wa kanuni hii, mpango huo waweza kuwa na vipengele vinavyohusu:
(a) mipango na uratibu wa ujenzi na matumizi ya majengo kwenye ardhi;
(b) uzoaji wa takataka katika ardhi;
(c) ulinzi na hifadhi ya maeneo yoyote ya hifadhi ya misitu kwenye ardhi ya kijiji, au kwenye maeneo mengine yenye misitu inayosimamiwa na kijiji, au kwenye maeneo mengine maalum ya ardhi ya kijiji;
(d) utoaji wa misaada kitaaluma ili kukisaidia katika usimamizi wa ardhi ya kijiji;
(e) kuchangia gharama za usimamizi wa ardhi ya kijiji pale ambapo gharama za usimamizi zimeongezeka kutokana na shughuli za maendeleo yanayotokea katika halmashauri ya wilaya au ya mamlaka ya mji;
(f) muda usiozidi miaka mitatu, ambapo mpango wa usimamizi wa pamoja utadumu;
(g) taratibu za kusuluhisha tofauti baina ya pande shiriki za Mpango wa usimamizi wa Pamoja.
SEHEMU YA V
DAFTARI LA ARDHI KIJIJI
36. Sehemu ya Daftari
Daftari litagawanywa katika sehemu zifuatazo–
(a) Sehemu A Cheti cha Ardhi ya Kijiji;
(b) Sehemu B Daftari la Hati;
(c) Sehemu C Daftari Bayana la Kutahadharisha.
37. Cheti cha Ardhi ya Kijiji
(1) Cheti cha Ardhi ya Kijiji kitakuwa katika fomu iliyowekwa katika Jedwali la Kwanza na itahifadhiwa katika sehemu tofauti ya Daftari.
(2) Kumbukumbu pekee zinazoweza kuingizwa kwenye Cheti cha Ardhi ya kijiji ni:
(a) marekebisho, anayoagiza Kamishna yafanywe, ili kuweka kumbukumbu za mabadiliko ya mipaka ya ardhi ya kijiji;
(b) kumbukumbu zinazoonyesha vipande vya ardhi viliyomegwa au vilivyoongezwa kwenye ardhi ya kijiji chini ya fungu la 4 na la 5 la Sheria;
(c) kumbukumbu zinazoonyesha maeneo ya ardhi ya kijiji yaliyotangazwa kuwa ardhi yenye madhara chini ya fungu la 6 la Sheria.
38. Daftari la Hati
(1) Daftari la Hati litakuwa ni Daftari lenye:
(a) kumbukumbu ya hatimiliki za kimila sehemu ya 1 ya Daftari la Hati;
(b) kumbukumbu ya hakimiliki zisizo asili sehemu ya 2 ya Daftari la Hati;
(c) kumbukumbu zote za uhamishaji na shughuli zinazohusiana na hakimiliki za kimila na hakimili zisizo za asili, ikiwa ni pamoja na ilani zozote zilizoingizwa kwenye daftari la Hati-Sehemu ya 3 ya daftari la Hati.
(2) Afisa atasajili kwenye sehemu husika ya Daftari la Hati kwa namna ilivyoelekezwa na Kanuni hizi nyaraka zote zilizowasilishwa kwake katika fomu zilizoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza.
39. Daftari Bayana la kutahadha risha
(1) Daftari Bayana la kutahadharisha litakuwa daftari lenye:
(a) nyaraka za kurejesha hakimiliki ya kimila;
(b) amri za kutekeleza ardhi;
(c) amri za kuhakilisha kwa muda hakimiliki ya kimila;
(d) taarifa zinazohusu kulipa au kutolipa kodi ya pango, kodi, faini na malipo mengine yapaswayo kulipwa kwa taasisi yoyote ya umma kwa kuhusiana na hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo asili au ya kukalia ardhi ya kijiji;
(e) nyaraka zinazoweka kumbukumbu za maelezo ya mpango wa usimamizi wa pamoja;
(f) kumbukumbu inayoweka uamuzi wa Mkutano wa Kijiji au Halmashauri ya Kijiji au chombo kingine chochote chenye mamlaka ya kuamua kwamba eneo la ardhi ya kijiji litahifadhiwa kwa ajili ya matumizi ya misitu, usimamizi wa wanyama pori au vinginevyo yametengwa kwa malengo ya hifadhi;
(g) kumbukumbu inayoweka uamuzi wa mkutano wa Kijiji kwamba sehemu ya ardhi ya kijiji imetengwa kama ardhi ya pamoja ya kijiji kwa mujibu wa fungu la 13 la Sheria.
(2) Afisa atasajili kwenye Daftari Bayana la kutahadharisha kwa namna ilivyoelekezwa na Kanuni Hizi, nyaraka zote zinazohusiana na masuala yaliyorejewa kwenye kanuni hii, zitakazowasilishwa kwake kwenye fomu zilizoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza.
40. Watu wanaostahili kuwasilisha nyaraka kwa ajili ya usajili
Waraka kwa ajili ya usajili sharti uwasilishwe na mtu anayedai maslahi kutokana na waraka huo, au mwakilishi wake, na Afisa anaweza kuhoji ili ajiridhishe na utambulisho na maslahi ya mtu anayewasilisha waraka au kama ni mwakilishi mamlaka yake.
41. Taarifa za Usajili
(1) Usajili utahusisha hatua ya Afisa kuweka kwenye jalada waraka uliotolewa kwa mujibu wa kanuni ya 13, na kumkabidhi mtu anayeleta waraka kwa ajili ya usajili nakala ya waraka huo (ambayo mtu yule anatakiwa kuleta) baada ya nakala hiyo kuthibitishwa na Afisa kwamba ni nakala halisi ya waraka huo.
(2) Saini ya Afisa kama ilivyoelezwa katika ibara (1) ya kanuni hii, kwenye nyaraka iliyosajiliwa na nakala yake, itakuwa ushahidi tosha wa usajili.
42. Utoaji wa namba na hifadhi ya nyaraka zilizosajiliwa
Afisa atatoa namba zinazofuatana kwa kila waraka unaohifadhiwa na kuwekwa kumbukumbu kwenye waraka inayoonyesha tarehe ya usajili na jina la mtu aliyewasilisha waraka huo na Afisa atahifadhi nyaraka katika sehemu husika za Daftari la Hati kwa mpangilio kadri anavyozipokea.
43. Kumbukumbu kimaandishi iliyoambatanishwa na waraka uliosajiliwa
Kumbukumbu iliyosainiwa na Afisa itaambatishwa kwenye kila waraka iliyosajiliwa ikinukuu maelezo mafupi ya usajili, kumbukumbu hiyo itakuwa ushahidi tosha wa awali kwamba waraka umesajiliwa kama ipasavyo.
44. Kitabu cha muhtasari
Afisa atatunza kitabu kitakachoweka muhtasari wa kumbukumbu zilizomo kwenye Daftari la Hati, na kwa kila cheti kitakachosajiliwa, ataingiza katika kitabu hicho namba ya usajili, jina la mwenye au wenye cheti, tarehe ya cheti na tarehe usajili na ukurasa tofauti wa kitabu hicho utatumika kuweka kumbukumbu zinazohusu cheti kilichosajiliwa.
45. Mwenye haki kutaarifiwa
(1) Mwenye hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo asili anayefanya uhamishaji au shughuli kwenye ardhi au mtu mwingine yeyote anayehusika kwenye shughuli hiyo, aweza katika kipindi cha miezi miwili cha kukamilisha shughuli hiyo, kuwasilisha kwa afisa nyaraka za ushahidi wa shughuli hiyo.
(2) Endapo shughuli yoyote ya ardhi matakiwa kupata kibali cha mwanandoa, ushahidi wa kimaandishi wa shughuli hiyo lazima uambatishwe na ushahidi wa kimaandishi wa kibali hicho au vibali hivyo vimetolewa.
46. Jukumu la Afisa kwenye shughuli za ardhi
Endapo ushahidi kimaandishi wa shughuli za ardhi unapelekwa kwa Afisa chini ya Kanuni ya 45 na mtu anayehusika na shughuli hiyo ya ardhi ambaye si mwenye hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo ya asili, basi Afisa
atampelekea taarifa yule mwenye hakimiliki kuhusu jambo hilo na hatachukua hatua zozote za kusajili shughuli hiyo ya ardhi mpaka mwenye hakimiliki au mwakilishi wake atoe ushahidi wa kutosha kwamba alijiingiza katika shughuli hiyo ya kibiashara kwa hiari yake na kwamba alijua kwa ufasaha matokea ya shughuli hiyo.
47. Shughuli za miliki za ardhi
(1) Afisa atawajibika–
(a) kujiridhisha kwamba nyaraka zote muhimu zinazohusiana na shughuli yoyote ya ardhi, zimewasilishwa;
(b) kuambatisha nakala ya ushahidi kimaandishi kuhusu shughuli ya ardhi inayohusika (itakayotolewa na mwenye hakimiliki ya kimila au mwenye hakimiliki isiyo asili) kwenye waraka unaohusiana nayo, na kuipa namba ya nakala hiyo;
(c) kuambatanisha kumbukumbu kimaandishi iliyosainiwa na Afisa kwenye waraka iliyorejewa katika ibara ya (b) hapo juu, ikinukuu kwa muhtasari yaliyomo kwenye shughuli ya ardhi, na kumbukumbu ambayo itakuwa ushahidi tosha wa awali kwa shughuli ya ardhi imesajiliwa ipasavyo;
(d) Kuandika kwenye ukurasa wa Kitabu cha Muhtasari ambapo kwa mujibu wa kanuni ya 37, kumbukumbu za waraka unaohusiana na shughuli ya ardhi husika zimewekwa zikionyesha namba ya usajili wa shughuli ya ardhi, tarehe ya shughuli ya ardhi na tarehe ya usajili shughuli ya ardhi.
(2) Afisa hatakuwa na uwezo wa kuambatisha ushahidi wowote kimaandishi kwa shughuli ya ardhi kwenye waraka uliyosajili, au kuingiza kwenye Kitabu cha Muhtasari, taarifa yoyote inayohusu shughuli ya ardhi, endapo ushahidi huo kimaandishi haukuambatishwa na vibali vilivyorejewa katika kanuni ndogo ya (2) ya kanuni ya 45 popote pale ambapo vibali hivyo vinatakiwa, na hatua yoyote ya Afisa kinyume cha hali itakuwa batili.
48. Kipaumbele
(1) Shughuli katika ardhi inayomilikiwa kwa waraka uliyosajiliwa zitakuwa na kipaumbele baina yao kwa mpangilio wa tarehe na saa zilipopata usajili kwa mujibu wa kanuni ya 42.
(2) Shughuli ya ardhi iliyosajiliwa kwa mujibu wa kanuni ya 42, itapewa kipaumbele juu ya shughuli nyingine ambayo haikusajiliwa, hata kama shughuli iliyosajiliwa ilikamilishwa, kabla au baada ya shughuli isiyosajiliwa.
49. Afisa aweza kukataa kusajili nyaraka
Afisa aweza kukataa kusajili au kuingiza katika Daftari waraka wowote kama:
(a) haikuandaliwa katika fomu iliyoainishwa au;
(b) fomu au waraka mwingine umeharibika kwa kuchanwa, kuchafuka, kufifia maandishi au kuharibika kiasi cha kutoweza kueleweka tena; au
(c) waraka huo unaonyesha kuongezwa maneno kati ya mistari ya waraka, au nafasi kuwa tupu, maneno kufutwa au kubadilishwa isipokuwa tu kama waliowasilisha nyaraka hizo wamesaini au wameweka majina yao kwa mkato mahali penye maneno yaliyoongezwa palipo patupu palipofutwa au kubadilishwa na katika hali hiyo Afisa ataingiza katika rejesta kumbukumbu ya maneno kuongezwa, mahah kuacha patupu, kufutwa au kubadilishwa.
50. Uwezo wa Afisa kusahihisha makosa
Endapo mtu yeyote atadai kuwepo kosa au upungufu ulifanyika kwenye usajili au upungufu kwenye daftari umesababishwa na udanganyifu au kosa Afisa akiridhika kuwa dai limethibitisha kikamilifu atasahihisha kosa hilo la upungufu au usajili.
51. Usajili hautaondoa kasoro au kuhalalisha
Usajili hautaondoa hitilafu yoyote katika waraka uliyosajiliwi au kuhalalisha waraka ambao vinginevyo usingekuwa halali isipokuwa tu kwa kiwango kinachokubalika kwa mujibu wa Sheria na Kanuni hizi.
52. Daftari laweza kukaguliwa na nakala kupatikana
Daftari laweza kukaguliwa na kuchunguzwa na mwombaji yeyote wakati wa saa za kawaida za kazi na nakala halisi zilizothibitishwa na Afisa kuwa nakala halisi za wowote uliosajiliwa au sehemu yake vinaweza kupatikana kama vikitakiwa, lakini waraka uliohifadhiwa kwenye daftari au ulioambatishwa kwenye waraka ulisajiliwa na kuhifadhiwa katika daftari hautaruhusiwa kuondolewa katika daftari.
53. Nyaraka mbadala ya iliyosajiliwa
Endapo waraka asili uliyosajiliwa umepotea, umechanika au umeteketea, Afisa aweza kuandaa nakala itakayokuwa na maelezo yote kutokana na taarifa katika kumbukumbu zote katika ofisini na vyanzo vingine.
54. Nakala ya wataka uliyosajiliwa
(1) Endapo nakala iliyosajiliwa imepotea, imechanika au imeteketea, Afisa aweza, kutokana na maombi ya mmilikaji au mkazi, yakiambatishwa na tamko rasmi kwenye fomu iliyoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi, kuandaa nakala yenye maelezo yote yaliyomo kwenye hati asili au hati mbadala iliyosajiliwa.
(2) Afisa atathibitisha kwenye nakala kwamba ni nakala ya waraka uliosajiliwa.
(3) Afisa atatangaza ombi hilo kwa gharama ya mwombaji na tangazo hilo litalolewa katika gazeti linalosomeka kwa wingi katika eneo hilo na nakala inayoombwa itatolewa kwa siku thelathini baada ya tangazo.
55. Kupatikana waraka uliyosajiliwa
(1) Endapo waraka asili uliyosajiliwa na kupotea ukipatikana, Afisa ataufanyia marekebisho na atafuta hati mbadala iliyosajiliwa.
(2) Waraka mbadala uliosajiliwa na kututwa utatunzwa katika masjala.
56. Kupatina nakala ya waraka uliosajiliwa
(1) Endapo nakala ya waraka uliosajiliwa na kupotea inapatikana, Afisa ataufanyia marekebisho kwa kuingiza taarifa mpya na kufuta nakala mbadala.
(2) Nakala mbadala iliyofutwa itatunzwa katika masjala.
57. Nakala ya waraka potevu uliosajiliwa
Endapo waraka wowote uliosajiliwa chini ya Kanuni hizi, nakala yake iliyothibitishwa na Afisa itakubalika katika ushahidi wa mambo yaliyomo mbele ya Mahakama zote Tanzania kwa kuzingatia tofati za haki na kisheria.
58. Nakala iliyothibitishwa ya waraka uliosajiliwa kukubalika katika kesi ya madai
Kila nakala iliyothibitishwa ya waraka wowote uliosajiliwa na inayoonekana kwamba imesainiwa na Afisa itapokeleka kama ushahidi katika kesi yoyote ya madai mbele ya Baraza au Mahakama bila uthibitisho wa usahihi wa nakala hiyo au usahihi wa saini hiyo, isipokuwa tu kama itadaiwa kwamba waraka asili umeghushiwa au kwamba nakala inayoonekana kusainiwa na Afisa in ya kughushi na siyo sahihi.
59. Matumizi ya nakala iliyothibitishwa ya waraka uliosajiliwa katika kesi za madai
Katika kesi ya madai, upande unaopendekeza matumizi ya nakala iliyothibitishwa ya waraka uliosajiliwa utatoa nakala ya waraka huo kwa upande mwingine na nakala hiyo itapokelewa katika ushahidi endapo Baraza au Mahakama itaridhika kwamba nakala imetolewa mapema kabla upande unaopinga kukagua daftari asili ilikopatikana nakala.
60. Muda wa Masjala kuwa wazi
Masjala itakuwa wazi kwa umma kwa siku, saa na muda kadri Halmashauri ya Kijiji itakavyoamua.
SEHEMU YA VI
USULUHISHI WA MASLAHI NA MIPAKA KATIKA ARDHI
61. Taarifa kwa pande zinazohusika
Kwa malengo ya fungu la 54 la Sheria, Kamati kwa mujibu wa fungu la 7(2) Sheria itatoa taarifa kwa kutumia fomu maalum iliyoainishwa katika Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi.
62. Kuweka mipaka
(1) Kamati itatembelea ardhi inayohusika na uamuzi wa maslahi na mipaka katika ardhi ikitafuta, ikibaini/ikithibitisha, ikiamua na kuweka mipaka ya ardhi.
(2) Katika kuweka mipaka, Kamati itatumia alama za mipaka ambazo kwa kawaida zinatumika kwenye maeneo husika, ikiwa ni pamoja na mipaka ya njia, mifereji, uzio katani na mimea mingine na mawe.
(3) Katika kuweka alama za mipaka, sehemu ya mzunguko, kona na mabadiliko mengine ya mwelekeo yatapewa umuhimu, na kati ya sehemu hizo alama zitawekwa kwa umbali ambao utaziwezesha kuonekana kwa urahisi alama moja baada ya nyingine.
63. Uthibitisho wa mipaka
Kamati, mwombaji, na angalau watu wazima wawili ambao ni wakazi wa eneo waliohudhuria ukaguzi wa ardhi, watathibitisha usahihi wa mipaka kwa kusaini katika fomu iliyoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi.
64. Kusafisha na kuweka alama kwenye mipaka
Gharama zinazohusiana na shughuli zilizotajwa katika Kanuni ya 61 ya Kanuni hizi zitalipwa na mwombaji au kama itakavyokubalika kati ya Halmashauri ya Kijiji na mwombaji.
65. Kutunza mipaka
Utunzaji wa mipaka utakuwa jukumu la wenye hakimiliki ya kimila.
66. Kipimo cha Upimaji
Kipimo cha upimaji kitakuwa mita.
67. Matavarisho ya Muhoro
(1) Katika utaratibu wa kuweka mipaka ya ardhi Kamati itaandaa mchoro wa ardhi inayohusika.
(2) Mchoro utapaswa–
(a) utachorwa na kuambatishwa na fomu iliyoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza la kanuni hizi;
(b) utachorwa kwenye karatasi inayodumu muda mrefu kwa kutumia kifaa cha kuandikia kitakachoweka alama ya kudumu;
(c) utakuwa wa mistari inayounganishwa na kufanya umbo lililofungwa;
(d) kuonyesha sambamba na mstari, umbali uliopimwa katika mita, kati ya alama moja na nyingine zilizochorwa kwa alama za msalaba;
(e) kuonyesha majina ya wakazi wa vipande vyote vya ardhi jirani;
(f) kuonyesha mwelekeo unaokaribia kaskazini;
(g) kuonyesha alama za rejea zinazoonekana na za kudumu kama zipo, kwenye ardhi au karibu, ikiwa ni pamoja na njia za miguu, barabara, mapito ya mifugo, mito, majengo ya kudumu, majabali na miti.
68. Taratibu za upimaji
(1) Mipaka itapimwa kwa kutumia futi kamba na haitakuwa lazima kuchora mchoro kwa vipimo au kubainisha ukubwa wa eneo.
(2) kama mwombaji anataka kujua ukubwa wa ardhi husika aweza kufanya taratibu na kulipa gharama za huduma ya Mpima Ardhi.
69. Kuweka kumbu-kumbu ya haki za njia
Haki ya njia itaonyeshwa katika mchoro kwa mistari ya nukta na itafafanuliwa wazi wazi.
70. Mgao wa mchoro
Kamati, itatayarisha nakala tatu za mchoro ambazo zitagawiwa kwa Kamati, mwombaji na Halmashari ya Kijiji.
71. Kumbu-kumbu za uamuzi wa ntaslahi na mipaka katika ardhi
(1) Kumbukumbu ya uamuzi wa maslahi na mipaka katika ardhi itatayarishwa kwa kila kipande cha ardhi ambacho kinahusika na dai moja au zaidi na itaonyesha:
(a) jina la mdai, au kama kuna zaidi ya mtu mmoja anayedai ardhi hiyo, majina ya wadai wote;
(b) aina na kiasi cha maslahi kinachodaiwa katika ardhi;
(c) kiasi cha ardhi kinachodaiwa;
(d) muda ambao au muda wanaodai maslahi katika ardhi hiyo;
(e) mahali na mipaka ya kipande husika cha ardhi;
(f) njia na mipaka ya Haki za njia zozote au Haki za fursa ya njia au huduma nyingine za umma zinazodaiwa kuwepo kwenye, juu au chini ya ardhi;
(g) Uamuzi wa Kamati ya Uamuzi ya Kijiji au kadri itakavyokuwa uamuzi wa Afisa Mshauri wa Uamuzi wa Kijiji kuhusu dai au madai hapo pamoja na maelezo kwa ufupi ya sababu za uamuzi huo.
(2) Kumbukumbu ya uamuzi wa maslahi katika ardhi na mipaka lazima iambatishwe na mchoro ulioandaliwa kwa mujibu wa kanuni ya 67.
(3) Kumbukumbu ya uamuzi wa maslahi ya ardhi na mipaka itakuwa kwenye fomu iliyoonyeshwa kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni Hizi.
72. Taarifa ya upimaji wa ardhi nayomilikiwa kwa hakimiliki ya kimila inayosajiliwa
(1) Endapo haki ya kumiliki ya kimila imetolewa baada ya uamuzi wa maslahi na mipaka ya ardhi, na baadaye ardhi ikapimwa, mkazi atatoa taarifa kwa Afisa wa eneo lililopimwa na kuwasilisha ramani iliyothibitishwa.
(2) Taarifa iliyotolea kwa mujibu wa kanuni ndogo ya kwanza itaandikwa kwenye fomu iliyoainishwa katika Jedwali la Kwanza la Kanuni Hizi.
73. Namba ya Uthitibisho wa Kipande cha Ardhi
Kipande cha ardhi ambacho, baada ya uamuzi wa maslahi na mipaka ya ardhi, hakimiliki ya kimila imetolewa na kusajiliwa katika Daftari la Ardhi ya Kijiji, kitaonyesha namba ya pekee ya Utambulisho wa Kipande cha Ardhi (UKA) itakayotolewa na Afisa.
74. Mgawanyo
Endapo kunafanyika mgawanyo wa hakimiliki ya kimila iliyosajiliwa, namba ya utambulisho ya awali (UKA) itafutwa na namba nipya ya utambulisho (UKA) itatolewa kwa kila eneo jipya litokanalo na mgawanyo, kwa kutumia fomu iliyoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi.
SEHEMU YA VII
MENGINI YO
75. Waziri aweza kuweka vya juu vya kumiliki ardhi
(1) Waziri aweza, kwa kuwasiliana na Waziri mwenye dhamana ya kilimo, kwa Amri iliyotangazwa kwenye Gazeti, kuweka kiwango cha juu cha ardhi ambacho mtu yeyote anaweza kukalia kwa hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo ya asili.
(2) Katika kutekelelza jukumu lake chini ya kanuni ndogo ya (1), Waziri atazingatia:–
(a) taarifa na miongozo yote inayopatikana kuhusu tathmini ya ardhi kuhusu matumizi maalum kwa mkulima mdogo, shughuli za ukulima, za ufugaji na za misitu katika sehemu na maeneno mbalimbali ya uchumi na kilimo Tanzania ili kusukuma maendeleo halisi ya ukulima na matumizi kamili ya ardhi;
(b) haja ya kuhimiza na kuhakikisha utunzaji wa mazingira;
(c) kuhusiana na ardhi itayotumika kwa maendeleo ya miji, miongozo iliyopo ya ukubwa wa viwanja kwa aina mbalimbali za uendelezaji wa miji kama ilivyoandaliwa na Idara va Mipango Miji;
(d) haja ya kusaza ardhi katika kila kijiji kwa ajili ya ugavi wa siku za usoni;
(e) mila na desturi zilizopo vijiini katika wilaya au mkoa ambako anapendekeza kuweka viwango vya juu vya ardhi kama mipaka ambayo mwanakijiji yeyote au famili itaruhusiwa kumiliki.
(3) Viwango vya juu tofauri vya ardhi vyaweza kuwekwa:
(a) kwa kila mkoa; na
(b) kila wilaya mkoani; na
(c) kila kijiji wilayani
(4) Viwango vya juu vinavyowekwa chini ya kanuni hii vitarejewa mara kwa mara na kurekebishwa inapobidi.
76. Taratibu za idhini ya viwango vya juu vya kumiliki ardhi
(1) Mpaka hapo matangazo yatakapotolewa na kutangazwa kwa mujibu wa kanuni ya 74, Halmashauri yoyote ya kijiji haitatoa au kukubali kutoa an kuidhinisha uhamishaji wa hakimiliki ya kimila au kutoa au kuidhinisha utoaji wa hakimiliki isiyo asili katika ardhi ya kijiji au hakimiliki ya kimila zaidi ya hekta ishirini au kiwango itakachomfanya mwanakijiji apate zaidi ya hekta ishirini au kiwango cha juu alichonacho mwanakijiji, bila idhini ya Halmashauri ya Wilaya au kamishna kwa mujibu wa Kanuni hii.
(2) Maombi yakipokelewa kwa Halmashauri ya kijiji ya kutoa ardhi au kwa hakimiliki ya kimila au kwa hakimiliki isiyo ya asili au ya kuidhinisha utoaji wa hakimiliki isiyo ya asili kwa kiwango cha hekta ishirini na moja (21) hadi hekta hamsini (50), Halmashauri ya kijiji itawasilisha maombi hayo kwenye Halmashauri ya Wilaya yenye mamlaka katika wilaya ambako kijiji kipo, pamoja na mapendekezo yake juu ya maombi hayo na haitaidhinisha maombi hayo isipokuwa kwa maandishi kwamba ameafiki maombi hayo.
(3) Maombi yakipelekwa kwa Halmashauri ya kijiji ya kutoa ardhi ama kwa hakimiliki ya kimila au kwa hakimiliki isiyo ya asili au ya kuidhinisha utoaji wa hakimiliki isiyo ya asili kwa kiwango kinachozidi hekta hamsini (50), Halmashauri ya kijiji itawasilisha maombi hayo kwa Kamishna pamoja na maendelezo yake juu ya maombi hayo na haitaidhinisha maombi hayo isipokuwa kwa maandishi kwamba imeafiki maombi hayo.
77. Misingi ya jumla ya usuluhishi
(1) Katika utekelezaji wa shughui za usuluhishi chini ya Sheria au Kanuni hizi, mtu aliyeteuliwa kutimiza majukumu chini ya fungu la 7 au kanuni ya 16, au Kamati katika kutekeleza majukumu yake chini ya fungu la 54, na halmashauri katika kutekeleza majukumu yake chini ya fungu la 14 na la 60 la Sheria–
(a) ataongozwa na misingi ya kutokuwa na upendeleo, usawa na haki, kwa kuzingatia, pamoja na mambo mengine, haki na wajibu wa pande zote, mila na sheria za Bunge na utamaduni nchi, na kwa kutia; maanani inavyopaswa vipengele vya Katiba ya nchi, na mazingira ya shauri pamoja na mahusiano na migogoro ya awali baina ya pande husika;
(b) wataendesha shughuli za usuluhishi kwa namna watakavyoona inafaa, kwa kuzingatia matakwa ya pande husika, mazingira ya mgogoro na umuhimu wa kufikia usuluhishi wa haraka wa mgogoro;
(c) watakuwa na kuwasiliana na pande husika mbalimbali au kwa pamoja;
(d) wakati wowote wa uendeshaji wa shauri watatoa mapendekezo kwa mdomo au kwa maandishi, kwa kutoa au bila kutoa sababu,
(e) kutokana na usuluhishi, inapodhihirika kwamba kuna vipengele vya mapatano au usuluhishi ambavyo vyaweza kukubalika na pande zote wataandaa dondoo za mapatano au usuluhishi na watawaeleza pande zote dondoo hizo, na baada ya kupokea maoni yao, watarekebisha dondoo kwa kuzingatia maoni hayo.
(2) Endapo mapatano au usuluhishi umefikiwa na pande zote, kamati au Halmashauri, kadri itakavyokuwa, watatayarisha mkataba wa maandishi, ambapo baada ya kusainiwa na pande zote, utawawajibisha wote.
(3) Mkataba wa maandishi utathibitishwa na msuluhishi aliyeteuliwa, na zilizothibitishwa za mkataba zitagawiwa kwa pande zote.
78. Maandalizi ya nyaraka
Afisa au Msajili wa Wilaya watasaidia katika kuandaa nyaraka na fomu kwa niaba ya halmashauri ya kijiji, Kamati, Halmashauri au mwombaji au mmiliki wa ardhi atakayetokea kutumia haki zake chini ya sheria, ili kurahisisha usuluhishi na usajili wa ugawaji na shughuli za kibiashara za maslahi katika ardhi.
79. Fomu zita-kazotumika kuhusiana na Sheria na Kanuni hizi
Fomu zilizoorodheshwa katika Jedwali la Kwanza ndizo fomu zinazopaswa kutumika kwa utekelezaji wa majukumu chini ya sheria na kanuni zinazorejewa nayo.
80. Mabadiliko ya fomu
Fomu zilizoorodhesliwa katika Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi zaweza kufanyiwa mabadiliko au marekebisho katika lugha ili kukidhi mahitaji ya kila shauri, na mabadiliko yoyote katika fomu ambayo hayagusi mambo ya msingi hayataathiri uhahali wake.
81. Ada
Ada zilizotajwa katika safu ya pili ya Jedwali la pili la Kanuni hizi ndizo zitakazokuwa ada zinazotakiwa kulipwa kwa ajili ya shughuli zozote zilizoorodheshwa katika safu ya kwanza ya Jedwali la Pili.
82. Faini
(1) Unapotokea uvunjaji wa masharti, kama ulivyoorodheshwa katika safu ya 2 ya Jedwali la Tatu la Kanuni hizi kwa hakikimali ya kimila, Halmashauri ya Kijiji inaweza kutoza faini kama ilivyoainishwa katika Jedwali la Tatu la Kanuni hizi.
(2) Halmashauri ya Kijiji itakuwa na uhuru wa kumtoza mkazi kiasi cha faini ambacho ni pungufu kuliko kilichoko kwenye jedwali lililotajwa.
83. Ushuhuda wa Kusaini Nyaraka
Ushuhuda na uandaaji wa nyaraka utafanyika kama ulivyoainishwa katika Fungu la 63 la Sheria ya Ardhi ya Mwaka na fungu 91 hadi 94 la Sheria ya Usajili wa Ardhi, Sura Na. 334.
JEDWALI LA KWANDA
FOMU
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 1
JAMHURI YA MUUGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AMRI YA KUITWA KWENYE KAMATI YA UAMUZI YA KIJIJI
(Chini ya fungu la 53)
Kwa: Bwana/Bibi/Bi 1 ........................................................................................ |
Mkutano wa Kijiji cha ........................................................................................... |
Umeidhinisha ombi kuhusu uamuzi kwa eneo maalum la ardhi lililoko ...................... |
linalokaribia takriban ......................................................... (ukubwa/eneo 2). |
Unaamuriwa kuhudhuriwa wewe binafsi na kutoa ushahidi wakati wa usikilizaji wa uamuzi wa |
eneo maalum la ardhi lililotajwa hapo juu. Shauri hilo litasikilizwa .............................. |
(mahali) siku ya .................................. tarehe .................. saa .............................. |
Tafadhali zingatia kwamba kutoa maelezo ya uongo katika ushahidi wako kunaweza kusababisha ufunguliwe mashtaka ya jinai. |
Jina la Saini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uamuzi ya kijiji ................................... |
Tarehe: ........................................................................................................... |
Imepokelewa na .............................................................................................. |
Saini: ............................................................................................................. |
Tarehe ........................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 2
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AMRI YA KUWASILISHA NYARAKA MBELE YA KAMATI YA KIJIJI
(Chini ya fungu la 53)
Kwa: Bwana/Bibi/Bi 1 ....................................................................................... |
Mkutano wa Kijiji cha ............................................... umeidhinisha ombi la kufanya |
uamuzi kwa eneo maalum lililoko ........................................... linalokaribia takriban |
............................................................. (ukubwa/eneo 2). |
Unaamriwa kuwasilisha nyaraka wewe binafsi au kupitia mwakilishi wako wakati wa kusikiliza madai yanayohusu uamuzi kwa eneo maalum la ardhi siku ya .................. |
Shauri litasikilizwa ............................................ (mahali) tarehe ........................... |
saa .................................................................................................................... |
Tafadhali zingatia kwamba kuacha, bila sababu za msingi kuwasilisha nyaraka zinazotakiwa kunaweza kusababisha mashtaka ya jinai yafunguliwe dhidi yako. |
Jina na Saini ya Mwenyekiti, Kamati ya Uamuzi ya Kijiji .................................... |
tarehe ................................................................................................................ |
Imepokelewa na ............................................................................................. |
Saini ............................................................................................................. |
Tarehe .......................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 3
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
WITO WA KUHUDHURIA MBELE YA KAMATI YA UAMUZI YA KIJIJI
(Chini ya fungu la 53)
Kwa: Bwana/Bibi/Bi 1 ....................................................................................... |
amewasilisha ombi kwa Halmashauri ya Kijiji cha ........................................... kwa |
ajili ya uamuzi wa eneo maalum la ardhi ambayo ameiombea hakimiliki ya kimila, lililoko |
...................................... linalokaribia takriban .................................. (ukubwa/eneo 2). |
Mkutano wa Kijiji cha .......................................................... umeamua kuanza utaratibu wa uamuzi kwa eneo maalumu la ardhi. Unatakiwa uhudhurie mbele ya kamati hiyo wewe |
binafsi tarehe ................................. saa ........................................ kueleza madai yako. |
Zingatia kwamba endapo hutafika bila sababu za msingi unaweza kuhesabiwa kwamba umefuta madai yako. |
Jina na Saini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uamuzi ya Kijiji ............................... |
Tarehe ......................................................................................................... |
Imepokelewa na ............................................................................................ |
Cheo ........................................................................................................... |
Tarehe ......................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 4
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
WITO WA KUHUDHURIA KUSIKILIZWA MBELE YA BARAZA LA ARDHI LA KIJIJI
(Chini ya fungu la 61)
Kwa: Bwana/Bibi/Bi 1 ....................................................................................... |
Unatakiwa uhudhurie mbele ya Baraza wewe binafsi siku ya ................................... |
tarehe .................................. saa .............................. kutoa ushahidi na kulisaidia |
Baraza katika suala la mgogoro kati ya ................................................................. |
na ...................................................................................................................... |
Tafadhali zingatia kwamba kutoa maelezo ya uongo katika ushahidi wako kunaweza kusababisha mashtaka ya jinai yafunguliwe dhidi yako. |
Jina ............................................................................................................... |
Saini: ............................................................................................................ |
Sifa: Mwitishaji Baraza la Ardhi la Kijiji cha ...................................................... |
Tarehe .......................................................................................................... |
Imepokelewa na ............................................................................................ |
Sifa: ............................................................................................................. |
Tarehe: ......................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 5
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KIAPO CHA SHAHIDI
{mprestriction ids="1,2,3"}
(Chin ya fungu la 56)
Mimi ...................................................................... ninaapa kwa dhati kwamba ushahidi |
nitakaotoa kuhusu suala lililoko mbele ya ................................................... (Kamati/Afisa), utakuwa kweli na kweli tupu na itakuwa kweli tu Mungu nisaidie. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 6
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUSUDIO LA KUTANGAZA ARDHI YENYE MADHARA
(Chini ya fungu la 6)
Kumb. Na. ......................... |
|
Mimi ..................................................................................... NINATOA TAARIFA kwamba ninakusudia kulitangaza eneo la ardhi lifuatalo kuwa ardhi yenye madhara: |
|
(a) Mahala eneo lilipo ................................................................................. |
|
(b) Mipaka na ukubwa wa eneo hilo ............................................................. |
|
(c) Sababu za kutoa tamko ........................................................................ |
|
Tamko litatolewa baada ya siku sitini (60) kuanzia tarehe ya kutangazwa taarifa hii kwenye Gazeti. Watu na mamlaka zote zitakazopewa taarifa hii zaweza kuwasilisha maelezo kwa Kamishna wa Ardhi kuhusiana na tamko lililopendekezwa maelezo ambayo inabidi yawasilishwe katika muda wa siku thelathini tokea tarehe ya kupewa taarifa hii. |
|
Imetolewa hapa ........................................................ siku ya ......................... |
|
tarehe ............................... mwezi wa .............................. mwaka 20 .................. |
|
......................................... |
|
Imepokelewa na ............................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha .......................................................... |
|
Tarehe .......................................................................................................... |
|
Wakazi kwenye ardhi yenye madhara inayopendekezwa |
|
Jina na saini/kidole gumba .............................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 7
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUITANGAZA ARDHI YENYE MADHARA
(Chini ya fungu la 6)
Kumb. Na. .......................... |
|
Mimi .............................................................................................................. |
|
(a) Mahala eneo lilipo ................................................................................. |
|
(b) Mipaka na ukubwa wa eneo hilo ............................................................. |
|
(c) Sababu za kutoa tamko ........................................................................ |
|
Taarifa itakuwa na nguvu za kisheria siku thelathini baada ya kutangazwa katika Gazeti. |
|
Zingatia: Tamko hili ni amri ya kutwaa ardhi iliyotajwa katika tamko hili Fidia italipwa kwa upotevu wowote utakaosababishwa na amri hii kwa mujibu wa Kanuni za Ardhi ya Vijiji. Unawajibika kuwasiliana na Afisa Mtendaji wa Kijiji kuhusu masuala yote yanayohusiana na tamko hili. |
|
KWA AMRI YA RAIS | |
.......................................... |
|
Imetolewa na: ................................................................................................ |
|
Jina na saini/alama ya kidole gumba cha mkazi ................................................ |
|
Tarehe ........................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 8
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA KUHAWILISHA ARDHI YA KIJIJI KUWA ARDHI YA KAWAIDA AU ARDHI YA HIFADHI
(Chini ya fungu la 4)
Kumb. Na............................ |
|
Mimi ............................................................................................................... |
|
(a) Mahala ................................................................................................ |
|
(b) Mipaka na ukubwa ............................................................................... |
|
(c) Sababu za uhawilisho .......................................................................... |
|
Uhawilisho waweza kufanywa siku tisini (90) baada ya kutangazwa kwa taarifa hii katika Gazeti. |
|
Mtu yeyote anayekalia ardhi yoyote ya kijiji inayoweza kuhawilishwa kwa mujibu wa taarifa hii aweza kupeleka kwa Kamishna wa Ardhi na Halmashauri ya Kijiji akieleza kwa nini eneo lake lisiwe sehemu ya eneo litakalohawilishwa au kwa nini eneo lote lililotajwa lisihawilishwe. |
|
Mtu yeyote atakayepatwa na upotevu kwa sababu ya pendekezo la uhamilisho aweza kuomba fidia kutoka kwa Kamishna wa Ardhi kwa kutumia fomu ya maombi yenye kichwa cha habari "OMBI LA MKAZI WA ARDHI KULIPWA FIDIA" |
|
Imetolewa hapa ................................. siku ya ............................ tarehe............... |
|
mwezi wa ................................................ mwaka 20 ......... |
|
........................................... |
|
Imepokelewa na sisi ......................................................................................... |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha ............................................................ |
|
Tarehe: ............................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 9
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA KUHAWILISHA ARDHI YA KIJIJI
(Chini ya fungu la 4)
Kumb. Na. ......................... |
|
UKA Na. ............................ |
|
Mimi .................................................................................................................. |
|
wa ...................................................................................................................... |
|
(a) Mahala ................................................................................................ |
|
(b) Mipaka na ukubwa ............................................................................... |
|
(c) Sababu za uhawilisho .......................................................................... |
|
Uhawilisho utakuwa na nguvu za kisheria siku thelathini baada ya tarehe ya kutangazwa kwake katika Gazeti. |
|
.......................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 10
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAMKO LA MGONGANO WA MASLAHI
(Chini ya fungu la 53)
Mimi .............................................................................................................. |
wa ................................................................... nikiwa mjumbe wa Halmashauri ya |
Kijiji/Mjumbe wa Kamati ya Halmashauri ................................................................ |
inayoshughulikia masuala ya ardhi katika kijiji cha .................................................. |
NATAMKA KWAMBA mimi binafsi/jamaa yangu wa karibu ...................................... |
(taja uhusiano) nina maslahi katika suala linalohusu ardhi kama ifuatavyo:– |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
(Aina ya mgongano wa maslahi na maelezo ya ardhi) |
Tamko limetolewa hapa ............................................. tarehe ................................ |
mwezi wa ..................................................... mwaka 20 ..................................... |
Saini ............................................................................................................. |
Imepokelewa na: ......................................................................... Mwenyekiti wa |
Tarehe: ......................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 11
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA KWA HALMASHAURI YA KIJIJI KUDAI FIDIA
(Chini ya fungu la 4 na la 6)
Kumb. Na. ......................... |
|
Mimi .................................................................................................................. |
|
wa................................................................... NINATOA TAARIFA kwamba Waziri |
|
(a) Mahali eneo lilipo .................................................................................. |
|
(b) Mipaka na ukubwa wa eneo ................................................................... |
|
ZINGATIA KWAMBA unayo haki ya kudai fidia kwa upotevu uliosababishwa na kuitangaza ardhi ya pamoja kuwa ardhi ya madhara/kuhahiwilisha ardhi ya pamoja. |
|
Madai yako lazima uyawakilishe kwangu katika kipindi kisichozidi siku 60 tangu ya kupokelewa taarifa hii. |
|
Imetolewa hapa ....................... siku ya ................. tarehe .............................. |
|
mwezi wa ........................................ mwaka 200 ................................................ |
|
........................................... |
|
Imepokelewa siku ya ....................................... ya tarehe ................................ |
|
mwezi wa ......................................... mwaka 200 ................................................ |
|
Mwenyekiti wa Kijiji ......................................................................................... |
|
Afisa Mtendaji wa kijiji .................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 12
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA HALMASHAURI YA KIJIJI YA KULIPWA FIDIA
(Chini ya fungu la 4 na 6)
Kumb. Na. ......................... |
|
1. Jina la Kijiji ........................................................................................... |
|
2. Wilaya kilipo Kijiji ................................................................................. |
|
3. Mahali ilipo ardhi ya pamoja inayohusika na madai .................................. |
|
4. Ukubwa/Eneo linakaribia takriban ........................................................... |
|
5. Matumizi ya sasa ya ardhi ..................................................................... |
|
6. Upotevu uliosababishwa na uhawilishaji ardhi/kutangazwa ardhi yenye madhara |
|
7. Taja haki za pamoja ambazo kwazo Halmashauri ya Kijiji inadai fidia na kiasi cha fidia inayodaiwa ........................................................................................... |
|
8. Ambatisha taarifa yoyote inayofafanua misingi ya madai ya fidia ................ ............................................................................................................. |
|
Tarehe .................................................................................................. |
|
Majina na Saini za wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji ................................ |
|
............................................................................................................. |
|
Tarehe .................................................................................................. |
|
Uamuzi wa Kamishna wa Ardhi: |
|
Sehemu zifuatazo za madai zimeidhinishwa (taja sehemu zilizoidhinishwa na toa sababu za kutoidhinishwa kwa sehemu zingine za madai). 2 |
|
........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
|
Madai yote yamekataliwa kwa sababu zifuatazo: 3 | |
.......................................................................................................................... .......................................................................................................................... .......................................................................................................................... .......................................................................................................................... .......................................................................................................................... |
|
Jina na Saini ya Kamishna wa Ardhi ..................................................................... |
|
Tarehe ............................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 13
JAMHURI YA MUUGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KIBALI CHA FIDIA
(Chini ya fungu la 4 na 6)
KWA: ................................................................................................................. |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
Maombi yako ya kulipwa fidia yamekubaliwa/yamekataliwa kwa misingi ifuatayo: |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
Kamishna wa Ardhi Afisa Mteule ........................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 14
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA KWA MKAZI WA ARDHI KUDAI FIDIA
(Chini ya fungu la 4 na 6)
Kumb. Na. ........................... |
|
Mimi ............................................................................................................... |
|
(a) Mahali: ................................................................................................. |
|
(b) Mipaka na ukubwa: ............................................................................... |
|
ZINGATIA: kwamba una haki ya kudai fidia kwa ajili ya upotevu utakaosababishwa na tamko la ardhi ya pamoja kuwa ardhi yenye madhara/uhawilishaji wa ardhi ya pamoja. |
|
Madai yako lazima yawasilishwe kwangu kupitia Halmashauri ya Kijiji katika siku sitini (60) tangu kupokelewa kwa taarifa hii. |
|
Kama utahitaji msaada wakati wa kujaza fomu hii ya madai, unaweza kuomba msaada kutoka kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji au mtu yeyote unayedhani anaweza kukusaidia. |
|
Imetolewa hapa ........................................ siku ya ........................................... |
|
tarehe .............................................. mwaka 20 .................................................. |
|
............................................ |
|
Imepokelewa hapa ..................................... siku ya leo ................................... |
|
tarehe ............................... mwezi .................. mwaka 20 ................................... |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya kijiji cha ............................................................ |
|
Tarehe ........................................................................................................... |
|
Wakazi wa Ardhi yenye madhara inayopendekezwa |
|
Jina na Saini/Kidole Gumba .............................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 15
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA MKAZI WA ARDHI KULIPWA FIDIA
(Chini ya fungu la 4 na 6)
1. Majina kamili (Jina la ukoo kwanza) |
(i) Jinsia .................................................................................................... |
(ii) Umri ...................................................................................................... |
2. Anwani: .......................................................................................................... |
3. Umeoa/umeolewa. Ndiyo/Hapana |
4. Watoto wanaoishi pamoja na wewe |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
5. Mahali ilipo ardhi inayohusika na fidia: |
Kijiji ............................................................................................................... |
Wilaya ........................................................................................................... |
6. Ukubwa wa eneo |
7. Matumizi ya sasa ya ardhi ............................................................................... |
8. Taja hasara zilizosababishwa na kuhawilishwa ardhi/tamko la ardhi kuwa ardhi yenye madhara. |
9. Taja haki ya ardhi inayohusika na fidia na kiasi cha fidia unachodai: 1 |
(a) Hakimiliki ya kimila ........................................................... Ndiyo/Hapana |
Kiasi kinachodaiwa ................................................................................ |
(b) Uboreshaji usiohamishika ................................................. Ndiyo/Hapana |
Kiasi kinachodaiwa ............................................................................... |
(c) Hakimiliki isiyo ya asili (taja aina) ........................................................... |
Ndiyo/Hapana |
(d) Gharama ya kuihama ardhi .............................................. Ndiyo/Hapana |
(e) Madai mengineyo kiasi kinachodaiwa (tafadhali toa maelezo kamili iwezekanavyo) |
............................................................................................................ |
............................................................................................................ |
............................................................................................................ |
Jina na saini/alama ya kidole gumba ya mwombaji au waombaji .............................. |
........................................................................................................................... |
Tarehe ................................................................................................................ |
Nakala kwa: Halmashauri ya Kijiji |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 16
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
CHETI CHA ARDHI YA KIJIJI
(Chini ya fungu la 7)
Kumb. Na. .......................... |
|
Leo tarehe ................................. ya mwezi .......................... mwaka 20............ |
|
Hii ni kuthibitisha kuwa Halmashauri ya kijiji (humu ikirejewa kama "Halmashauri") cha |
|
............................................................... katika Wilava ya .................................. |
|
(i) Halmashauri itasimamia ardhi ya kijiji kadri ya sheria za mila zinazohusu ardhi kwenye eneo nusika; |
|
(ii) Halmashauri italinda mazingira kwa kuhifadhi rutuba ya ardhi na kuzuia mmomonyoko wa udongo; |
|
(iii) Halmashauri italinda haki za njia; |
|
(iv) Halmashauri italinda na kutunza mipaka ya kijiji; |
|
(v) Halmashauri itatunza na kukihihiifadhi kwa usalama cheti hiki; |
|
(vi) Endapo mipaka ya kijiji imebadilishwa au kurekebishwa, Halmashauri itatuma cheti kwa Kamishna ili kuidhinisha mabadiliko au marekebisho ya mipaka kwenye cheti; |
|
(vii) Halmashauri itatoa cheti cha hakimiliki ya kimila na kutunza daftari la ardhi ya pamoja. |
|
(viii) Endapo mipaka ya kijiji imebadilishwa, Halmashauri itatuma cheti kwa Kamishna ili kuidhinisha mabadiliko au marekebisho hayo ya mipaka kwenye cheti; |
|
(ix) Halmashauri itatoa cheti cha hakimiliki ya kimila na kutunza daftari la ardhi ya pamoja. |
JEDWALI
(Maelezo kamilil ya ardhi na mipaka ya jumla)
IMETOLEWA na Rais na imekabidhiwa kwa MKONO wangu na LAKIRI rasmi kuwekwa siku na mwaka vilivyoandikwa hapo juu. |
|
LAKIRI | |
.......................................... |
|
LAKIRI halisi ya Halmashauri ya kijiji cha .......................................................... |
|
1. Jina: .................................................... | Saini ................................. |
Cheo: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji.............................................. |
|
Anuani: .......................................................................................... .......................................................................................... |
|
2. Jina: .................................................... | Saini ................................. |
Cheo: Katibu wa Halmashauri ya kijiji..................................................... |
|
Anuani: ............................................................................................... ........................................................................................................... |
|
ADA | |
Nakala: Msajili |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 18
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA HAKIMILIKI KIMILA
(Chini ya fungu la 22)
SEHEMU YA I: (Ijazwe na mwombaji/waombaji) |
1. Jina la Mwombaji: |
A. Jina/Majina Kamili ya Mwombaji/waombaji: |
(Ongezea itakavyolazimu) |
B. Majina kamili ya wana familia ya Mwombaji (Jina la Familia Kwanza) |
C. Jina la chombo au taasisi inayoleta maombi |
(Angalau wajumbe wawili wa familia wawasilishe maombi) |
(Ongeza itakavyolazimu) |
Jaza kifungu kinachoendana na ombi lako |
2. Anuani (kama kawaida si mkazi kijijini) |
............................................................................................................. ............................................................................................................. |
3. Uraia .................................................................................................... |
4.1 Kuoa/kuolewa ....................................................................................... |
1. Watoto na miaka (Inahusika na kifungu A na B hapo juu) ............................................................................................................ |
5. Mahili ilipo ardhi inayoombwa |
Eneo ndani ya Kijiji:................................................................................ |
............................................................................................................ |
Kijiji:...................................................................................................... |
Wilaya:.................................................................................................. |
6 |
7. Matumiza ya ardhi kwa sasa hivi (kama vile kilimo, ufugaji, makazi) ............................................................................................................. ............................................................................................................. |
8. Matumizi yanayopendekezwa au yanayokusudiwa katika ardhi (kama ni tofauti na inavyotumiwa hivi sasa). ............................................................................................................. ............................................................................................................. |
9. (a) Unataka kumiliki ardhi kama familia? Ndiyo/Hapana. |
(b) Unataka kumiliki ardhi kama ya jumuiya? Ndiyo/Hapana. |
(c) Unataka kumiliki ardhi kama ya mtu/watu binafsi Ndiyo/Hapana. |
Eleza maslahi kwenye ardhi (mgawanyo au asilimia) kama unataka kumiliki ardhi kwa pamoja au kwa pamoja na mgawanyo wa hisa. |
Saini/kidole gumba cha mwombaji:.................................................................... |
Angalau wanafamilia wawili kwa kijadi; au maafisa wateule wawili wa chombo, lazima waweke saini kwanye ombi. |
Tarehe ya ombi................................................................................................ |
SEHEMU YA PILI:(kwa matumizi ya ofisi tu) |
Maoni na mapendekezo ya Halmashauri ya Kijiji/Halmashauri ya Wilaya: |
...................................................................................................................... ...................................................................................................................... ...................................................................................................................... ...................................................................................................................... |
Majina na Saini ya Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji. |
............................................................................. tarehe................................. |
............................................................................. tarehe................................. |
............................................................................. tarehe................................. |
............................................................................. tarehe................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 19
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AHADI YA TOLEO YA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya fungu la 24)
Kumb. Na ............................ |
||
KWA: .................................................................................................................. ............................................................................................................................ |
||
YAH: MAELEZO YA ARDHI (Pamoja na mahali, ukubwa/eneo) |
||
............................................................................................................................. ............................................................................................................................. |
||
Ombi lako la Hakimiliki ya Kimila (humu ikirejewa kama Hakimiliki) juu ya eneo lililoelezwa hapo juu limeidhinishwa kwa vipengele na masharti ya Hakimiliki kama ifuatavyo:– |
||
(i) Kipindi: bila kikomo/miaka ........................ tangu .............................. |
||
(ii) Kodi ya pango, kama ipo, ni ........................ kwa mwaka iwezayo kurejewa katika kipindi kisichopungua miaka mitano. upya baada ya kila miaka kumi |
||
(iii) Matumizi: ardhi itatumika kwa (taja hapa matumizi. kwa mfano kilimo na/au ufugaji). |
||
(iv) Utawajibika kuhakikisha kwamba mipaka ya ardhi inadumu kuwa bayana kipindi chote cha Hakimiliki. |
||
2. | Maelezo yafuatayo yanahitajika: | |
(a) Majina yako kamili kwa herufi kubwa. (Maombi ya cheti cha hakimiliki ya kimila kutolewa kwa jina la mtu au watu ambao si waombaji hayatafikiriwa). |
||
(b) Kama ni kwa madhumuni ya wanandoa. |
||
(c) Anwani yako kamili ya makazi |
||
(d) Onyesha: |
||
(i) Kama unataka kumiliki peke yako Hakimiliki |
||
(ii) Kama unataka kumiliki hakimiliki kwa pamoja bila mgawanyo wa hisa, kama si wanandoa, idhini ya Mahakama lazima ipatikane kwanza; |
||
(iii) Kama unataka kumiliki kwa pamoja kwa hisa, taja kiwango cha hisa za kila mmoja wenu. |
||
3. | Malipo yafuatayo yalipwe wakati wa kukubali ahadi |
|
Malipo ya mbele........................................................................................... |
||
Ada ya cheti cha Hakimiliki .......................................................................... |
||
Ada ya Usajili ya Kijiji .................................................................................. |
||
Ushuru wa Serikali kwenye cheti na nakala kama inahusika ............................ |
||
Kodi ya pango toka .............................................hadi .................................. |
||
4. | Kiasi cha fedha kilichoonyeshwa hapo juu kilipelekwa kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji au maafisa wateule (Stakabadhi asili ziletwe kwangu pamoja na) maelezo yaliyotajwa hapo juu. |
|
5. | Ahadi hii itakuwa wazi kwa kipindi cha siku tisini (90) tangu tarehe utakapoipokea. Kama unataka kukubali ahadi hii, basi jaza fomu Na. 20 iitwayo "KUKUBALI TOLEO LA HAKIMILIKI YA KIMILA". |
|
Wako Mtiifu |
||
Majina na Saini .................................................................................................... |
||
............................................................ |
|
|
Jina na Saini ........................................................................................................ |
||
.................................................................. |
Muhuri wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 20
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KUKUBALI AHADI YA TOLEO LA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya fungu Ia 24)
Kumb.Na ............................ |
>Mimi/Sisi ........................................................................................................ |
nakubali/tunakubali kupokea hakimiliki ya kimila kwa vipengele na masharti yaliyomo kwenye |
ahadi ya toleo la vipengele ya kimila ya tarehe......................................................... |
Jina/Majina na saini .............................................................................................. |
Tarehe.................................................................................................................. |
Picha |
>Ada |
vipengele ya kimila ya tarehe |
............................................................................................................................. |
............................................................................................................................. |
Jina/Majina na saini ............................................................................................... |
Tarehe................................................................................................................... |
Picha |
Ada |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 21
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
CHETI CHA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 25)
Hati ya Kijiji Na ........................................ |
Leo tarehe ....................................... mwezi ..................................... 20 .............. |
(i) Mkazi/Wakazi watalipa kodi ya mwaka ya Shs ......................... kabla ya tarehe ................. ya mwezi .................... 20 ................ kila mwaka (kama inahusika). |
(ii) Ardhi itatumika kwa ajili ya .................................................................... |
(iii) Mkazi/Wakazi watawajibika kuhifadhi mazingira (ardhi na maji). |
(iv) Mkazi/Wakazi watahakikisha kwamba mipaka ya ardhi inalindwa na kutunzwa pia kuhakikisha bayana kwa kipindi chote cha hakimiliki. |
(v) Mkazi/Wakazi wataheshimu na kuhifadhi haki za njia zilizopo. |
(vi) Uhakilishi wa hakimiliki kwa mtu yeyote au kikundi chochote cha watu ambao kwa kawaida si wakazi wa kijiji lazima uidhinishwe na Halmashauri ya Kijiji. |
JEDWALI |
||
(Maelezo kamili ya eneo na mipaka yake) |
||
Jina ........................................................... | Muhuri wa Jina .................. |
|
Saini ......................................................... | Halmashauri Wadhifa: Khatibu wa |
|
Wadhifa: Mwenyekiti wa Halmashauri | Halmashauri |
|
Anuani | Anuani ............................. |
|
Tarehe: .................................. | Tarehe: ............................ |
|
2. | Saini/kidole gumba la mkazi ..................................................................... |
|
Lakiri | Jina: ................................ |
|
Saini: ............................... |
||
Wadhifa: Afisa Ardhi wa Wilaya |
||
ZlNGATlA Kanuni ya 83 kuhusu Ushohuda wa Kusaini Nyaraka. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 22
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA NAKALA YA CHETI CHA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 57)
Kwa: Afisa Mtendaji wa Kijiji | |
Mimi/Sisi, mkazi/wakazi niliyesajiliwa chini ya haki ya kimila yenye UKA Na. .......... |
|
kwenye kitabu cha Muhtasari Na. .......................................................................... |
|
Ninaomba itolewe nakala ya Cheti ya Hakimiliki ya Kimila ambayo nakala yake anapotoa/ imeharibika/imechafuliwa 1. |
|
TAMKO | |
Mimi/Sisi tunathibitisha kwamba yaliyotamkwa hapo juu ni kweli kadri ya ufahamu na imani yangu. |
|
Jina na Saini ya mmilikaji wa Hakimiliki ardhi ya kimila aliyesajiliwa |
|
Tarehe: ................................................................................................................ |
|
Tamko limetolewa mbele yangu, Jina na Saini |
|
................................................................ | ....................................... tarehe |
................................................... Afisa Mtendaji wa Kijiji |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 23
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KULIPA KODI
(Chini ya Fungu la 28)
Kumb Na. ................. |
|||
UKA Na. ................... |
|||
Kwa: Jina la Mkazi |
|||
UNATAARIFIWA KWAMBA katika kipindi kisichozidi siku kumi na nne (14) tangu tarehe ya taarifa hii unatakiwa kulipa kiasi cha Shs ..................................... ikiwa ni kodi ya pango kwa hakimiliki ya kimila kama inavyofafanuliwa hapa chini:– |
|||
(i) | Kodi inayodaiwa kwa | Shs. | ..................... |
(ii) | Malipo ya awamu sehemu Kodi inayodaiwa ........................ | Sh. ................ |
|
(iii) | Adhabu (Kama ipo) .......................................... | Shs | ...................... |
JUMLA | .................................. |
||
ZINGATIA: Endapo huitikii kwa kuitekeleza taarifa hii, nakala ya taarifa itawasilishwa kwenye Mahakama Mamlaka yenye mamlaka katika eneo la Kijiji cha ................................... |
|||
Jina na saini ......................................................................................................... |
|||
Imetolewa kwa: |
|||
Jina na saini |
|||
....................................................................... | tarehe | ................................... |
|
.................................................... | Mkazi |
||
Tafadhali fika na fomu hii unapokuja kulipa kodi yako. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 24
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA UHAKILISHAJI WA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 30)
Kwa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha ...................................................... |
Mimi/Sisi ..............................................................TUNAKUTAARIFU kwamba nina/ |
MAELEZO YA ARDHI |
UKA (Kama ipo) |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
Tarehe ya kutolewa hakimiliki ya kimila ................................................................. |
KUTOKANA NA UPENDO NA HUBA ASILI KIASI CHA YA SHS. |
............................................................................................................................ |
Mimi/Sisi ....................................................................................... M/Wahakilishaji, |
tunahakilisha wa .................................................................................................... |
.................................................................. Mhakilishwi kwa kipindi kilichosalia cha |
hakimiliki ya kimila iliyotolewa kwangu/kwetu. |
AIDHA MIMI/SISI * ................................................................................................... |
M/Wahakilishwaji na tunaomba kusajiliwa kama M/Wahakilishwi wa Hakimiliki ya kimila kwa vipengelena masharti yaliyokwisha wekwa kwenye hakimiliki hiyo. |
1. IMESAINIWA NA KUTOLEWA na |
............................................................................................................................. |
.....................................................................................................(MHAKILISHAJI) |
Sahihi ................................................................................................................ |
Wadhifa ............................................................................................................. |
Anuani ............................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
2. IMESAINIWA NA KUTOLEWA na |
3. Ninayemfahamu binafsi/alietambulishwa kwangu na |
...................................................................................................(MHAKILISHAJI) |
ambaye namfahamu binafsi leo tarehe........................mwezi..................20............ |
Shahidi |
Sahilii ................................................................................................................ |
Sifa: .................................................................................................................. |
Anuani ............................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 25
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KUKUBALIWA/KUKATALIWA KWA UHAKILISHAJI WA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 30)
Kwa: ................................................................................................ Jina/Majina |
Kwa: ................................................................................................ Jina/Majina |
Mimi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha .................................. kwa niaba ya Halmashauri ya Kijiji NAKUBALI/NAKATAA uhakilishaji hakimiliki ya kimila ambayo maelezo yake yamefafanuliwa katika fomu hii. |
Sababu za kukataaa uhakilishaji (rejea kifungu cha 30(4) cha Sheria ya Ardhi ya Vijiji): |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
.......................................................................................................................... |
Jina na saini ............................................................. tarehe .............................. |
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha ............................................................... |
Jina na saini ............................................................... tarehe.............................. |
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha .................................................................................. |
Imetolewa kwangu/kwetu ............................................ tarehe ............................. |
Saini ya M/Wahakilishi ............................................... tarehe ............................. |
Sahihi ya M/Wawakilishaji .......................................... tarehe.............................. |
Nakala ya fomu hii lazima itumwe kwa Kamishna wa Ardhi |
ZINGATIA: FOMU HII INAWAHUSU WATU AMBAO KWA KAWAIDA SI WAKAZI WA KIJIJI |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 26
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA KIBALI CHA KUTOA HAKIMILIKI ISIYO ASILI
(Chini ya Fungu la 31)(5)
Kumb. Na. ........................ |
|
UKA. ................................ |
|
SEHEMU YA I |
|
MIMI/SlSI .......................................................................................................... |
|
NINAOMBA/TUNAOMBA IDHINI ya kutoa hakimiliki isiyo asili kutokana na hakimiliki ya kimila iliyosajiliwa katika daftari la kijiji kwa rejea iliyotajwa hapo juu: |
|
1. Aina ya uhamishaji |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
2. Maelezo yanayohusu anayepewa hakimiliki isiyo asili: |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
Saini ya mwombaji/waombaji |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
.......................................................................................................................... |
|
Tarehe: .............................................................................................................. |
SEHEMU YA II |
|
Kwa Matumizi ya Ofisi tu |
|
ZINGATIA: Kama maombi haya ni kwa ajili ya upangishaji, lazima urejee fungu la 2(5) cha Sheria ya Ardhi ya Vijiji ujue namna ya kuishughulikia na tumia aya ya pili hapo chini kwa maombi ambayo si upangishaji. |
|
Kwa maombi ambayo si upangishaji |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa. |
|
(b) Sababu za kukataliwa |
|
.................................................................................................................. |
|
.................................................................................................................. |
|
................................................................................................................... |
|
................................................................................................................... |
|
.................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
.................................................................................................................. |
|
Tarehe: ...................................................................................................... |
|
2. | Kwa maombi ya upangishaji |
Ombi la Daraja A: Kifungu cha 32 (5) (a) |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa: |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
.................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
|
................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
................................................................................................................. |
|
Tarehe: ..................................................................................................... |
|
Ombi la Daraja B: Kifungu cha 32 (5)(b) |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa: |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
Saini ......................................................................................................... |
|
Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
|
................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Tarehe: ..................................................................................................... |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa na Mkutano wa kijiji |
|
(b) Sababu za kukataliwa |
|
................................................................................................................. |
|
................................................................................................................. |
|
Imesainiwa kwa niaba ya Mkutano wa Kijiji ................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Mkutano wa Kijiji |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
.................................................................................................................. |
|
Tarehe: ...................................................................................................... |
|
Ombi la Daraja la C: Kifungu cha 32 (5)(c) |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa: |
|
.................................................................................................................. .................................................................................................................. .................................................................................................................. .................................................................................................................. |
|
Saini ......................................................................................................... |
|
Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
|
.................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Tarehe: ...................................................................................................... |
|
(a) Ombi limekubaliwa/limekataliwa na Mkutano wa Kijiji |
|
(b) Sababu za kukataliwa |
|
................................................................................................................. ................................................................................................................. |
|
Imesainiwa kwa niaba ya Mkutano wa Kijiji ................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Mkutano wa Kijiji |
|
Imetolewa kwangu/kwetu ................................................................................................................. |
|
Tarehe ...................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 27
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI 1999
(SURA YA 114)
CHETI CHA KIBALI CHA HAKIMILIKI ISIYO
ASILI (UPANGISHAJI/LESENI/HAKI YA MATUMIZI)
Chini ya Kifungu cha 31 (9))
Kumb. Na. ........................ |
|
UKA. Na. .......................... |
|
1. Halmashauri ya Kijiji cha ....................................................................... katika |
|
Wilaya ya ........................................................................................................... |
|
INATOA KIBALI cha ............................................. (taja aina ya hakimiliki isiyo asili) |
|
iliyotolewa na ..................................................................................................... |
|
.......................................................................... wa ......................................... |
|
kwa ................................................................................ wa ............................> |
|
......................................................................................................................... |
|
2. Ufafanuzi kamili wa ardhi na mipaka ya jumla: |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
3. Ukubwa/Eneo la ardhi ni takriban: .................................................................... |
|
4. Makisio ya ukubwa/eneo la ardhi linalotolewa hakimiliki isiyo asili (kama ni tofauti na ilivyotajwa hapo juu katika kifungu cha 3). |
|
Jina:............................................Muhuri/ | Jina ................................... |
Saini:.........................................Lakiri | Saini:.................................. |
Sifa: Mwenyekiti ya Kijiji | Sifa: Afisa Mtendaji |
wa Halmashauri | |
ya Kijiji | |
Sahihi/Kidole gumba cha mpokeaji | |
........................................................................................................................... |
|
Tarehe |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 28
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA KUPEWA HAKIMILIKI ISIYO ASILI
KATIKA ARDHI YA KIJIJI
(Chini ya Fungu la 32)
Kumb. Na ......................... |
|
SEHEMU YA I |
|
Mimi/Sisi ........................................................................................................... |
|
NINAOMBA/TUNAOMBA kupewa hakimiliki isiyo asili kwenye ardhi ya kijiji yenye kumbukumbu iliyotajwa hapo juu: |
|
1. Aina ya hakimiliki isiyo asili ........................................................................ |
|
2. Maelezo ya Mwombaji wa Hakimiliki isiyo asili |
|
..................................................................................................................... |
|
..................................................................................................................... |
|
Saini |
|
.................................................................................................... (waombaji) |
|
Tarehe .......................................................................................................... |
|
SEHEMU YA II |
|
ZINGATIA ILANI: Kama ombi hili ni la upangishaji rejea fungu la 32(5) cha Sheria ya Ardhi ya Vijiji ili ujue namna ya kulishughulikia, kuhusu maombi ya upangishaji, angalia kipengele cha 2 hapo chini; |
|
1. Kwa maombi yasiyo ya upangishaji |
|
(a) Limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa: |
|
.......................................................................................................................... |
|
.......................................................................................................................... |
|
.......................................................................................................................... |
|
Saini .................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Saini ................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
2. Kwa maombi ya upangishaji |
|
Ombi la Daraja la A: fungu la 32(5)(a) |
|
(a) Limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa ............................................................ |
|
Sahihi:............................................................................................ |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Sahihi: .............................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
(a) Limekubaliwa/limekataliwa na Mkutano wa Halmashauri ya Kijiji |
|
(b) Sababu za kukataliwa ........................................................... |
|
Saini ............................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Tarehe: .......................................................................................... |
|
Saini: ............................................................................................ |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Limetolewa kwangu/kwetu |
|
Saini: ........................................................................................... |
|
Mwombaji/Waombaji |
|
Tarehe: ........................................................................................ |
|
Ombi Daraja B: fungu la 32(5)(b) |
|
(c) Limekubaliwa/limekataliwa na Mkutano wa Kijiji |
|
(d) Sababu za kukataliwa: |
|
..................................................................................................... |
|
Imesainiwa kwa niaba ya Mkutano wa Kijiji |
|
Mwenyekiti wa Mkutano wa Kijiji |
|
Tarehe: .......................................................................................... |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
Saini ya mwombaji/waombaji | |
Tarehe: .......................................................................................... |
|
Ombi la Daraja C: fungu la 32(5)(c) |
|
(a) Limekubaliwa/limekataliwa |
|
(b) Sababu za kukataliwa ...................................................................................................... |
|
Saini: ............................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Saini: ............................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
(c) Limekubaliwa/limekataliwa na Mkutano wa Kijiji |
|
(d) Sababu za kukataliwa: |
|
....................................................................................................... |
|
Imesainiwa kwa niaba ya Mkutano wa Kijiji |
|
Mwenyekiti wa Mkutano wa Kijiji |
|
Tarehe: ......................................................................................... |
|
Ushauri wa Kamishana wa Ardhi ..................................................... |
|
Saini ............................................................................................. |
|
Tarehe ........................................................................................... |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
Saini ya mwombaji/waombaji ........................................................... |
|
Tarehe: .......................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 29
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KUTOLEWA KWA HAKIMILIKI ISIYO ASILI
KWENYE ARDHI YA KIJIJI (PANGO/LESENI/HAKI YA MATUMIZI)
(Chini ya Kifungu cha 32(9))
Kumb. Na.: .......................... |
|
UKA Na.: ............................. |
|
1. Halmashauri ya Kijiji cha .......................................................................... katika |
|
Wilaya ya ............................................................................................................ |
|
INATOA (taja aina ya hakimiliki isiyo asili) katika ardhi ya kijiji kwa .................................................... wa ..................................... ................................................. (humu ndani anarejewa kama "mpokeaji") kwa kipindi cha miaka/miezi/wiki 1 .................................... kuanzia tarehe .............. 20 ............ |
|
(i) kwa utolewaji wa pango/leseni a u haki ya matumizi, mpokeaji atalipa maliSpo ya mbele T.Shs. ........................................................................... |
|
(ii) kwa utolewaji wa pango/leseni au haki ya matumizi, mpokeaji atalipa kodi ya pango kwa mwaka/mwezi/wiki 2 ya T.Shs. |
|
.......................................tarehe au kabla ya tarehe............................... ya kila mwaka/mwezi/wiki 3. |
|
(iii) Mpokeaji ataitunza na kuiweka ardhi katika hali bora. |
|
(iv) upangishaji wowote wa hakimiliki isiyo asili utahilaji kibali cha Halmashauri ya Kijiji na ridhaa ya Mkutano wa Kijiji |
|
(v) Taja masharti mengine yoyote ......................................................... |
|
1. Ufafanuzi kamili wa ardhi na mipaka yake ya jumla: ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
|
2. Ukubwa/Eneo la ardhi ni takriban: ...................................................................... |
|
3. Ukubwa/eneo la ardhi inayotolewa hakimiliki isiyo asili (kama ni tofauti na aya ya 3 hapo juu) |
|
Jina: ....................................................... Muhuri | Jina ................................. |
Saini: ........................................................... | Saini ............................... |
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji | Afisa Mtendaji wa Kijiji |
ZINGATIA: Kama kuna makubaliano au mkataba kuhusiana na hakimiliki isiyo asili, |
|
nakala iambatishwe. |
|
Imekubaliwa kwa Azimio la Mkutano wa Kijiji ulioketi tarehe ................................... |
|
Jina: .................................................................................................................. |
|
Saini: ................................................................................................................ |
|
Sifa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Anwani: ............................................................................................................. |
|
Mapendekezo ya Kamishna wa Ardhi: ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
|
Saini: .................................................................................................................. |
|
Tarehe: ............................................................................................................... |
|
Saini: Mpokeaji/Wapokeaji ................................................................................... |
|
Tarehe: ............................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 30
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KUREJESHWA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Kifungu cha 35)
Kumb. Na. ........................ |
|
UKA Na. ........................... |
|
Kwa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha ...................................................... |
|
1. Mimi/Sisi ........................................................ wa ......................................... |
|
......................................................................................................................... ......................................................................................................................... ......................................................................................................................... ......................................................................................................................... |
|
2. Natamka/tunatamka kwamba: |
|
(i) Urejeshaji haulengi kumnyang'anya mwanamke yeyote haki za makazi au haki yoyote nyingineyo chini ya sheria za kimila, ambayo kama si urejeshaji huu wa ardhi angestahili kuwa nayo; |
|
(ii) Madhumuni au matokeo ya urejeshaji si ya udanganyifu, si ukosefu wa udanganyifu na wala si kumnyang'anya mtu yeyote hakimiliki isiyo asili kinyume cha Sheria; |
|
(iii) Nitaendelea/tutaendelea kuwajibika na ukiukaji wowote wa masharti uliotokea kabla ya tarehe ya urejeshaji; |
|
(vi) Nitaendelea/tutaendelea kuwajibika kulipa riba itokanayo mkopo wowote niliochukua/tuliochukua kwa dhamana ya hakimiliki hiyo, na kulipa kodi, ushuru, ada ya malipo yaliyopaswa kulipwa hadi wakati wa urejeshaji |
|
(v) Watu wote wenye hakimiliki isiyo asili kwenye hakimiliki ya kimila wana taarifa ya urejeshaji huu na wameafiki kwa maandishi kwa kusaini hapa chini: |
|
Jina ..................................................................................... |
|
Saini .................................................................................... |
|
Tarehe .................................................................................. |
|
Jina ...................................................................................... |
|
Saini .................................................................................... |
|
Tarehe .................................................................................. |
|
1. Wategemezi wangu/wetu wanayo taarifa ya urejeshaji huu na wameafiki kwa maandishi kusaini hapa chini: |
|
Jina ...................................................................................... |
|
Saini ..................................................................................... |
|
Tarehe ................................................................................... |
|
Jina ....................................................................................... |
|
Saini ...................................................................................... |
|
Tarehe .................................................................................... |
|
(Ongeza majina zaidi ya wategemezi ikibidi) |
|
Kwa Matumizi ya Ofisi Imeandikwa kwenye Daftari la Ardhi la Kijiji leo tarehe .................................. ya mwezi ................................................ mwaka ................................... 20 ..................... |
|
Jina ..................................................................................... |
|
Saini .................................................................................... |
|
Sifa: Afisa Ardhi Mtendaji wa Kijiji |
|
Jina ...................................................................................... |
|
Saini ..................................................................................... |
|
Tarehe ................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 31
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
BARUA YA ONYO
(Chini ya Kifungu cha 38)
Kumb. Na. ........................ |
|
UKA Na. ........................... |
|
Mimi ................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha ..................................................... /Afisa |
|
Mteule ............................................................................................................... |
|
NINAKUTAHADHARISHA kwamba umevunja sharti/masharti ya hakimiliki ya kimila (ambayo imesajiliwa katika kumbukumbu za daftari la kijiji) kama ifuatavyo |
|
(1) ................................................................................................................ |
|
(2) ................................................................................................................ |
|
unashauriwa kama ifuatavyo:– |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
......................................................................................................................... |
|
imetolewa Tarehe .................. ya mwezi .............. wa .............. mwaka 20 .......... |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji/Afisa Mteule |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
......................................................................................................................... |
|
Mkazi/wakazi |
|
Tarehe ............................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji No. 32
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
KIBALI KWA HATUA YA HALMASHAURI
YA KIJIJI
(Chini ya Fungu la 39)
Kwa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha.......................................................... |
Wilaya ya.............................................................................................................. |
Mimi........................................................................................................Kamishna |
wa Ardhi wa........................................................................................................... |
NAIDHINISHA hatua inayopendekezwa na Halmashauri ya kijiji cha............................ |
Kumnyang'anya..........................................................................................wa kijiji cha ............................................................................................................................. |
Hakimiliki yake kimila kwa mujibu wa desturi za kimila zinazotumika kijijini kutokana na ukiukaji wa mara kwa mara wa masharti ya kumiliki hakimiliki hiyo ya kimila. |
IDHINI hii inatolewa kwa masharti yafuatayo: ........................................................................................................................... |
Imesainiwa........................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 33
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUJIELEZA
(Chini ya Fungu la 40)
Kumb. Na. ......................... |
|
UKA Na. ............................ |
|
Kwa: ........................................................................................................................... |
|
wa S. L. P. .......................................................................................................... |
|
NINAKUTAKA utoe maelezo kwanini usitozwe faini ya T.Shs. ..............................kwa |
|
1. ...................................................................................................................... ...................................................................................................................... |
|
2. ....................................................................................................................... ...................................................................................................................... |
|
Imetolewa hapa.........................................................leo tarehe...........................ya |
|
mwezi wa...........................................mwaka 200...........................................Saini |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha................................................./Afisa Mteule |
|
Imetolewa kwangu/Kwetu |
|
Mkazi/wakazi ...................................................................................................... |
|
tarehe ................................................................................................................. |
|
tarehe ................................................................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 34
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
ILANI YA KULIPA FAINI
(Chini ya Fungu la 40)
Kumb. Na. .......................... |
|
UKA Na. ............................. |
|
Kwa......................................................wa S. L. P. .............................................. |
|
UNATAARIFIWA kwamba Halmashauri ya Kijiji, baada ya kutafakari hoja zako kwa nini usilipe faini kutokana na ukiukaji wa masharti yaliyomo kwenye hakimiliki yako ya Kimila/hakimiliki isiyo ya asili 1, imeamua ulipe faini, na hivyo basi UNAAGIZWA kulipa faini ya shilingi ........................................................................ kwa sababu umekiuka masharti yafuatayo: |
|
1. ..................................................................................................................... |
|
2. ..................................................................................................................... |
|
Hatua zaidi zitachukuliwa dhidi yako iwapo faini hiyo haitalipwa katika siku thelathini (30) tangu taarifa hii kutolewa kwako. |
|
Imetolewa hapa.............................. leo tarehe......................................... ya mwezi |
|
Saini: .................................................................................................................. |
|
Sifa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji/Afisa Mteule |
|
Imetolewa kwangu/kwetu | |
Mkazi/Wakazi .................................................................................................. |
|
Tarehe ............................................................................................................. |
|
Tarehe.............................................................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 35
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUREKEBISHA KUKIUKA MASHARTI
(Chini ya Fungu la 41)
Kumb. Na. .......................... |
|
UKA Na. ............................. |
|
KWA: Jina....................................................................................................... Anuani: ................................................................................................. |
|
UNATAARIFIWA kwamba umekiuka masharti hali ambayo unatakiwa kurekebisha katika muda ulioonyeshwa hapa chini (taja ukiukaji na muda wa kurekebisha) |
|
1. .................................................................................................................. |
|
2. .................................................................................................................. |
|
Imetolewa hapa............................................leo tarehe...........................ya mwezi |
|
Jina: .................................................................................................................. |
|
Saini: ................................................................................................................. |
|
Sifa: Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji/Afisa Mtendaji wa Kijiji |
|
Tarehe ............................................................................................................... |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
Jina la Mkazi/wakazi............................................................................................. ........................................................................................................................... |
|
Saini.................................................................................................................... |
|
Tarehe.................................................................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 36
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AMRI YA USIMAMIZI
(Chini ya Fungu la 42)
Kumb. Na. ......................... |
|
UKA Na. ............................ |
|
KWA: .............................................................................................................. .............................................................................................................. |
|
UNATAARIFIWA kwamba baada ya Halmashauri ya Kijiji kuzingatia mazingira yote kuhusu ukiukaji wako wa masharti ya hakimiliki yako ya kimila pamoja na hoja ulizozitoa, imeamua kutoa AMRI YA USIMAMIZI kwako ili kuhakikisha kwamba unarekebisha masharti uliyokiuka katika kipindi kilichotajwa hapa chini (taja masharti yaliyokiukwa na muda wa ukiukaji yanayotakiwa kurekebishwa na muda): |
|
1. ....................................................................................................................... |
|
2. ....................................................................................................................... |
|
3. ...................................................................................................................... |
|
(ongeza kama ni lazima) |
|
Ukiukwaji huo utasimaniwa na................................................................................ |
|
Jina na Sifa za Afisa amayehusika........................................................................... ............................................................................................................................ |
|
Unawajibika kukamilisha hatua zilizotajwa katika AMRI YA USIMAMIZI katika kipindi cha siku sitini (60) au muda mrefu zaidi kwa kadri afisa anayekusimamia atakavyoamua. |
|
Saini..................................................................................................................... |
|
Tarehe................................................................................................................... |
|
Sifa....................................................................................................................... |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha................................................................... |
|
Imetolewa kwangu/kwetu |
|
Mkazi/wakazi......................................................................................................... |
|
Tarehe................................................................................................................... |
|
Tarehe................................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 37
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUREKEBISHA KUKIUKA MASHARTI OMBI LA IDHINI YA UHAKILISHWAJI KWA MUDA
(Chini ya Fungu la 43)
Kumb. Na. .......................... |
|
UKA Na. ............................. |
|
KWA: Kamishna wa Ardhi Halmashauri ya Kijiji cha................................................. |
|
INATAARIFU KWA Kamishna wa Ardhi kwamba mkazi wa ardhi iliyotajwa hapo juu kwa muda mrefu ameshindwa kurekebisha ukiukaji wa yafuatayo (taja makosa na hatua zilizochukuliwa) chini ya masharti ya hakimiliki ya kimila:– ........................................................................................................................... |
|
TUNAOMBA RUHUSA ya kuhakilisha kwa muda hiyo hakimiliki ya kimila. |
|
Tarehe..................................................mwezi wa ..................mwaka 20............... |
|
Jina na saini......................................................................................................... |
|
Tarehe................................................................................................................. |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha................................................................. |
|
Jina na saini......................................................................................................... |
|
Tarehe ................................................................................................................. |
|
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha..................................................................................... |
|
Lakiri/Mhuri wa Halmashauri ya Kijiji |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 38
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA UHAKILISHWAJI WA MUDA WA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 43)
Kumb. Na. ......................... |
|
UKA Na. ............................ |
|
KWA: Jina ..................................................................................................... Anuani.................................................................................................. |
|
UNATAKIWA kujieleza kwanini hakimiliki ya kimila unayomiliki isihakilishwe kwa mtu mwingine kwa kipindi cha miezi/miaka...........................(taja muda inayokusudiwa) kutokana na uvunjaji wa masharti yafuatayo yanayokupa fursa ya kukalia ardhi kwa hakimiliki ya kimila: |
|
1. ...................................................................................................................... |
|
2. ...................................................................................................................... |
|
Lazima uijibu taarifa hii katika kipindi cha siku....................tangu siku uliyokabidhiwa taarifa hii. |
|
Jina/Saini ............................................................................................................. |
|
Jina/Saini ............................................................................................................. |
|
Imetolewa kwangu/kwetu ............................................................................................................................. |
|
Tarehe ................................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 39
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AGIZO LA MASHARTI YA UHAKILISHAJI
KWA MUDA
(Chini ya Fungu la 43)
Kwa: (Jina la Mkazi/Wakazi) ......................................................................................................................... |
Eneo (na UKA Na. ya hakimiliki ya kimila kama ipo) ......................................................................................................................... |
Kijiji cha ............................................................................................................ |
Wilaya ya .......................................................................................................... |
TAARIFA INATOLEWA kwamba kwa sababu ya hii AMRI YA MUDA YA UHAKILISHAJI KWA MUDA, hakimiliki yako/yenu inahakilishwa kwa muda kwa (taja jina la mhakilishaji) |
HURUHUSIWI KUINGILIA USIMAMIZI AU MATUMIZI YA ARDHI HIYO WAKATI IKIWA CHINA YA UDHIBITI WA MTU/WATU WALIOTAJWA KATIKA AGIZO HILO |
Saini: ................................................................. Lakiri/Mhuri wa Halmashauri ya |
Kijiji .................................................. Tahere ..................................................... |
Sifa ................................................................................................................... |
Mweyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
Saini: ................................................................................................................. |
Sifa .................................................................................................................... |
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
Saini: ................................................................................................................. |
Tarehe ................................................................................................................ |
Tarehe ................................................................................................................ |
Imtolewa kwangu/kwetu: ........................................................................................................................... |
Mkazi/Wakazi ..................................................................................................... |
Tarehe ................................................................................................................ |
Tarehe ................................................................................................................ |
Mhakilishwaji |
Masjala ya Ardhi |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 40
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
LESENI YA MAKAZI
(Chini ya Fungu la 43)
Kwa: (taja Jina la Mkazi) .......................................................................................................................... .......................................................................................................................... |
Eneo (UKA Na. ya hakimiliki ya kimila kama ipo) .......................................................................................................................... |
Kijiji Cha............................................................................................................. |
Wilaya ya........................................................................................................... |
KWA LESENI HII YA MAKAZI UNARUHUSIWA |
kukaa kwenye ardhi iliyohakilishwa kwa muda kwa.................................................. |
(taja jina la Mhakilishaji).........................................................................kwa mujibu |
wa Agizo la uhakilishaji wa muda uliokabidhiwa tarehe..............................ya mwezi |
Masharti ya leseni hii ya makazi ni kama ifuatavyo:– |
1. Hutakiwi kuingilia usimamizi wa ardhi iliyowahilishwa kwa muda kwa ............................................................. (taja jina mthakilishwi kwa muda) |
2. Endapo unakusidia kupanda zao lolote katika ardhi unayokalia kwa leseni hii, unapaswa kufuata masharti na vipengele vyote vinavyoambatana na hakimiliki ya kimila kwa ardhi ambayo sehemu yake unakusudia kulima. |
3. Unapaswa kutekeleza maagizo yote unayopewa na mtu ambaye ardhi hiyo imehakilishwa kwake kwa muda. |
4. (ongeza kama inabidi) ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
Saini: .................................................................................................................. |
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji cha |
Tarehe ................................................................................................................. |
Saini: ................................................................................................................... |
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha...................................................................................... |
Tarehe................................................................................................................... |
Imetolewa kwangu/kwetu ........................................................................................ |
Mkazi/Wakazi ........................................................................................................ |
Tarehe ...................................................................................................................> |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 41
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KUBAINI UTEKELEZAJI ARDHI
(Chini ya Fungu la 45)
Halmashauri ya Kijiji cha...........................................................................kwenye |
kikao kitakachofanyika.......................................................saa............................ |
tarehe......................................ya mwezi wa.................................mwaka 20........ |
ikiwa ni kipindi kisichopungua siku 30 tangu tarehe ya taarifa hii, itajadili iwapo ardhi |
iliyopo..............................................................................ambayo inamilikiwa kwa |
hakimiliki ya kimila na.......................................................................................... |
(taja mmilikaji/wamilikaji) ya kijijini hapo limetekelezwa. |
MTU YEYOTE AMBAYE MWENYE MASLAHI KWENYE ARDHI HIYO ANAKARIBISHWA KWENYE KIKAO HICHO ILI AELEZEE HOJA ZAKE KWA NINI ARDHI HIYO ISITANGAZWE KUWA IMETELEKEZWA |
Jina/ Saini: ....................................................................Lakiri/Mhuri (Mhuri wa Kijiji) |
Sifa: Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
Jina/Sahihi: .......................................................................................................... |
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
Nakala kwa |
Kamishna wa Ardhi |
Jina: .................................................................................................................... |
Saini: ................................................................................................................... |
Tarehe: ................................................................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 42
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SHERIA YA ARDHI YA VIJIJI, 1999
(SURA YA 114)
AMRI YA UTEKELEZAJI ARDHI
(Chini ya Fungu la 45)
Halmashauri ya kijiji cha | |
............................................................................................................. INATOA TAARIFA |
|
kwamba baada ya kutafakari kwa makini hoja zote zilizotolewa katika kikao cha Halmashauri ya Kijiji kilichofanyika tarehe .....................................................................................mwezi |
|
wa ...........................................................20 ..........Halmashauri ya Kijiji imeazimia kwamba eneo linalomilikiwa kwa hakimiliki ya kimila kama ilivyoelezwa hapa chini limetelekezwa na hivyo basi inatoa AMRI YA MUDA YA UTEKELEZWAJI inayotangaza kwamba eneo limetelekezwa |
|
1. Mahali eneo lilipo: ........................................................................................... |
|
2. Ukubwa na mipaka ya ardhi ........................................................................................................................... |
|
3. Jina/Majina ya mkazi /wakazi: .................................................................................................... ........................................................................................................................... |
|
4. Sababu za kuamua kwamba ardhi/imetelekezwa: ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
|
Jina na sahihi ............................................................(Mhuri wa Halmashauri ya Kijiji) |
|
Tarehe ................................................................................................................ |
|
Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji | |
Jina na sahihi: ..................................................................................................... |
|
Tarehe ................................................................................................................ |
|
Katibu, Halmashauri ya Kijiji |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 43
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
OMBI LA KIBALI KUHUSU SHUGHULI YA ARDHI INAYOZIDI
KIWANGO CHA ARDHI KWA INAYOZIDI KIJIJI
(Chini ya Kifungu cha 18(2))
SEHEMU YA I: (Ijazwe na Halmashauri ya Kijiji) |
Mimi................................................................... Mwenyekiti wa Halmashauri ya |
Kijiji cha ..................................................................................katika Wilaya ya |
.......................................NINAOMBA KIBALI kwa shughuli ya ardhi iliyotajwa katika fomu hii. |
Kutolewa kwa hakimiliki ya kimila 1 |
Uhakilishaji wa hakimiliki ya kimila 2 |
Upangishaji wa hakimiliki ya kimila 3 |
Upangishaji kwenye ardhi ya Kijiji 4 |
(Taja shughuli nyingine yoyote ya ardhi ambapo mtu anayeruhusiwa kufidia ardhi atakalia ardhi inayozidi kiwango cha ardhi kwa kijiji) |
1. Jina kamili la mwombaji/waombaji binafsi (anza na jina la familia) |
(i) .................................................................................................... |
Jinsia/umri..................................................................................... |
(ii) .................................................................................................... |
Jinsia/umri..................................................................................... |
2. Anuani (kama kwa kawaida simkazi/wakazi kijiji)/eneo katika Kijiji .................................................................................................................... |
3. Nimeoa/Nimeolewa: .................................................................................................................... |
4. Watoto na umri wao:....................................................................................... |
5. Mahali ilipo ardhi inayoombwa: Eneo ndani ya |
Kijiji............................................................................................................... |
Wilaya ya: ..................................................................................................... |
6. Ukubwa/Eneo la ardhi ni takriban:...................................................................... |
7. Kiwango cha ardhi kinachozidi kiwango cha ardhi kwa Kijiji ambalo mwombaji atatakiwa kama kibali kitatolewa: ........................................................................................................................... |
8. Matumizi ya ardhi ya sasa k.m. ukulima, ufugaji, ujenzi wa nyumba:...................... ............................................................................................................................ ........................................................................................................................... |
9. Matumizi ya ardhi yanayopendekezwa (kama ni tofauti na matumizi ya sasa) ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
Sahihi/Kidole gumba cha mwombaji/waombaji ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
Sababu za mwombaji kuomba ardhi inayozidi kiwango cha ardhi kwa Kijiji (ajaze Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
Hoja za Halmashauri ya Kijiji kuunga mkono ombi (ijazwe na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kijiji): ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... ........................................................................................................................... |
Sahihi: ................................................................................................................ |
Mwenyekiti, Halmashauri ya Kijiji |
Sahihi: ............................................................................................................... |
Afisa Mtendaji wa Kijiji |
Tarehe: ............................................................. |
(Ongeza ikibidi) |
3. Majina ya watu wenye haki au maslahi kwenye ardhi au kutumia ardhi kwa malengo yoyote |
(i) ...................................................................................................... |
(iii) ...................................................................................................... |
(iii) ...................................................................................................... |
(Ongeza kama ikibidi) |
Jina na sahihi/kidole gumba cha mwombaji/waombaji |
Tarehe: ................................................................................................................ |
SEHEMU YA II |
|
A. Uamuzi wa Halmashauri ya Kijiji |
|
................................................................................................................ |
|
Majina na saini za Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji |
|
Tarehe: ..................................................................................................... |
|
B. Uamuzi wa Mkutano wa Kijiji (unapohusika) |
|
Majina na saini za Mwenyekiti wa Mkutano wa Kijiji na Afisa Mtendaji wa Kijiji. |
|
Tarehe: ..................................................................................................... |
|
C. Uamuzi wa Halmashauri ya Wilaya (unapohusika) |
|
Ombi limekubaliwa/limekataliwa kwa sababu ................................................ |
|
................................................................................................................ |
|
................................................................................................................ |
|
................................................................................................................ |
|
Jina na saini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya |
|
................................................................................................................ |
|
Tarehe: ..................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 44
[Imefutwa.]
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 45
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
PENDEKEZO LA UAMUZI NGAZI YA KIJIJI
(Chini ya Fungu la 51)
1. | Halmashauri ya Kijiji cha............................................................................. |
|
Wilaya ya ................................................................................................. |
||
INAPENDEKEZA kwa Mkutano wa Kijiji kwamba taratibu za uamuzi ngazi ya |
||
Kijijini zitumike kuhusu ardhi yote/sehemu maalum ya ardhi ya kijiji |
||
2. | Maelezo ya ardhi |
|
Mahali:..................................................................................................... |
||
Kijiji:........................................................................................................ |
||
Ukubwa/eneo la ardhi ni takriban................................................................ |
||
3. | Majina ya wakazi |
|
(i) ............................................................................................................ |
||
(ii) ............................................................................................................ |
||
4. | Majina ya watu wenye haki au maslahi kwenye ardhi au wanaotaka kuitumia ardhi hiyo kwa lengo lolote: |
|
(i) ............................................................................................................ |
||
(ii) ............................................................................................................ |
||
5. | Sababu za pendekezo:............................................................................... |
|
................................................................................................................ |
||
6. | Taratibu za zitakazofuatwa: |
|
................................................................................................................ |
||
................................................................................................................ |
||
Jina ............................... LAKIRI.........................................Jina:......................... |
||
Saini.....................................AU.............................................Saini..................... |
||
Mwenyekiti wa | MUHURI | Afisa Mtendaji wa |
Tarehe: .......................................... | Tarehe:................. |
|
Nakala kwa Kamishna wa Ardhi |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 46
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA KAMATI YA UAMUZI YA KIJIJI KUSIKILIZA MASUALA YA ARDHI
(Chini ya Fungu la 54)
Mkutano wa Kijiji cha ..................................................................................... umekubaliwa |
matumizi ya za uamuzi ngazi ya kijiji kwa ardhi iliyopo.......................................................... |
......................................................................................................................................... |
.............................................................(ENEO LA UAMUZI) |
Kamati ya uamuzi ya kijiji itafanya maamuzi maalum juu ya ardhi hiyo |
TAARIFA INAYOTOLEWA KWAMBA MKUTANO UTAFANYIKA |
(MAHALI) .....................................TAREHE ........................................... SAA.................... |
NA WATU WOTE MWENYE MASLAHI NDANI AU KARIBU NA ARDHIHIYO WANATAKIWA KUHUDHURIA NA KUWASILISHA MADAI YAO |
PIA ZINGATIA: |
Mtu yeyote mwenye madai ya kukalia ardhi kwenye ENEO LA UAMUZI lazima aonyeshe bayana alama za mipaka ya kipande au kiwanja cha ardhi kabla ya tarehe ya mkutano uliotangazwa kwa taarifa hii |
Saini:.............................................................................................................. |
Sifa Mwenyekiti wa Kamati ya Uamuzi ya Kijiji |
Tarehe............................................................................................................ |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 47
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
UTHIBITISHO WA MIPAKA
(Chini ya Fungu la 65)
Mkoa | Wilaya | Kijiji | UKA. Na. | Jalada Na. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Jina la Mkazi:......................................................................................................... |
Mahali ardhi ilipo:.................................................................................................... |
Mchoro (usiochorwa kwa vipimo):.............................................................................. |
Maelezo ya haki za njia na haki zingine za kutumia ardhi (kama zipo) |
Sisi tuliosaini hapa chini tunathibitisha kwamba mipaka iliyowekwa na kuonyeshwa kwenye mchoro ni sahilii kwa kadri ya ufahamu wetu wote: |
1. Mkazi/Mkazi: Jina..............................Sahihi.................................................. |
........................................................................................................................... |
........................................................................................................................... |
4. Wenye haki za njia na haki za |
........................................................................................................................... |
matumizi mengineyo............................................................................................. |
5. Mashahidi ............................................................................................................................ |
6. Wajumbe wa Kamati ya uamuzi ya Kijiji |
............................................................................................................................ |
Tarehe.................................................................................................................. |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 48
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
TAARIFA YA UPIMAJI WA MIPAKA YA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 65 na Kanuni ya 71)
Mkoa | Wilaya | Kijiji | Mahali | UKA Na. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Taarifa inatolewa kwamba ardhi iliyotajwa hapo juu imepimwa kwa mujibu wa Ramani ya Upimaji Na.............................................Nakala halisi ya Ramani ya Upimaji imeambatishwa. |
Jina la Mkazi:........................................................................................................ |
Saini:.................................................................................................................... |
Tarehe................................................................................................................... |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 49
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
KUGAWANYA HAKIMILIKI YA KIMILA
(Chini ya Fungu la 65 na Kanuni ya 74)
Mkoa | Wilaya | Kijiji | Mahali | UKA Na. |
Jina la Mkazi/Wakazi waliosajiliwa |
Mchoro (Usiochorwa kwa vipimo) |
Jina la Mwombaji/waombaji.................................................................................... |
UKA Na......................................................................................................(mpya) |
Maelezo ya haki za njia na haki zingine za kutumia ardhi (kama zipo):– Sisi tulioweka sahihi zetu hapa chini tunatamka kwamba mipaka iliyowekwa na kuonyeshwa kwenye mchoro ni sahihi kwa kadri ya ufahamu wetu wote. |
1. Mwombaji/Waombaji.............................Jina........................Sahihi..................... |
2. Mkuu wa familia (panapokuwa na mirathi)........................................................... |
3. Mashahidi........................................................................................................ |
4. Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji |
Tarehe:................................................................................................................ |
Fomu ya Ardhi ya Vijiji Na. 50
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria ya Ardhi ya Vijiji, 1999
(SURA YA 114)
KUMBUKUMBU YA UAMUZI WA MASLAHI NA MIPAKA YA ARDHI
(Chini ya Fungu la 54)
Eneo la Uamuzi..................................................................................................... |
||||||||
Kijiji...................................................................................................................... |
||||||||
Wilaya................................................................................................................. |
||||||||
Na. | Tarehe | Saa | Mahali na mipaka ya ardhi | Jina la Mdai | Maslahi yanayo- | Kiwango cha ardhi kinacho- | Muda ambao mdai amekalia ardhi | Maelezo ya haki za umma au jumuiya juu ya ardhi |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Ambatisha mchoro wa eneo la uamuzi wa maslahi na mipaka katika ardhi unaoonyesha mipaka na vipande vya ardhi vilivyoamuliwa |
JEDWALI LA PILI
ADA
(Kanuni ya 81)
Na. | Shughuli | Fungu/ Kanuni | Ada(Shilingi) |
1. | Ombi la hakimiliki ya kimila kwa mtu binafsi au familia (FAV. Na. 18)............................................................. | 22 | 500/= |
2. | Ombi la hakimiliki ya kimila kwa shirika, Chama cha Ushirika au kundi lolote halali la kijamn (FAV. Na. 18)............................................................................ | 22 | 2,5000/= |
3. | Ombi la kibali cha kutoa hakimiliki isiyo asili Upangishaji (FAV Na. 16).............................................................. | 31 | 500/= |
4. | Ombi la kutoa kibali cha hakimiliki siyo asili Leseni (FAV Na. 26)....................................................................... | 31 | 500/= |
5. | Ombi la kutoa kibali cha hakimiliki isiyo asili Haki ya matumizi (FAV. Na. 26)............................................... | 31 | 500/= |
6. | Ombi la kibali cha hakimiliki isiyo asili kuwekwa rehani......................................................................... | 31 | 1,000/= |
7. | Ombi la kibali ya hakimiliki isiyo asili ambayo si upangishaji, leseni na haki ya matumizi........................ | 32 | 750/= |
7. | (a) Ombi la kupewa hakimiliki isiyo asili kwenye ardhi ya kijiji (FAV Na. 28)................................................... | 32 | 1,000/= |
8. | Ombi la Daraja A kwa Halmashauri ya Kijiji la kupewa pango (FAV. Na. 28).................................................... | 32(5)(a) | 1,000/= |
9. | Ombi la Daraja B kwa Halmashauri ya Kijiji la kupewa pango (FAV. Na. 28).................................................... | 32(5)(b) | 1,000/= |
10. | Ombi la Daraja C kwa Halmashauri ya Kijiji la kupewa pango (FAV. Na. 28).................................................... | 32(5)(c) | 1,000/= |
11. | Kuingiza kumbukumbu ya hakimiliki ya kimila katika sehemu ya 1 ya Daftari la Hati la Daftari la Ardhi ya Kijiji........................................................................... | 21 Kanuni ya 38 | 1,000/= |
12. | Kuingiza kumbukumbu ya hakimiliki isiyo ya asili katika sehemu ya II Daftari la Hati la Daftari la Ardhi la Kijiji........................................................................... | 21 Kanuni ya 38 | 750/= |
13. | Kuingiza kumbukumbu ya uhamishaji au shughuli inayohusu hakimiliki ya kimila au hakimiliki isiyo asili au shughuli nyingine yoyote isiyotajwa katika sehemu ya 3 ya Daftari la Hati la Daftari la Ardhi ya Kijiji.................... | 21 Kanuni ya 38 | 750/= |
14. | Kuingiza tahadhari katika Daftari la Ardhi ya Kijiji........... | Kanuni 36 | 750/= |
15. | Upekuzi wa Daftari la Ardhi ya Kijiji................................ | Kanuni 52 | 1,000/= |
16. | Nakala iliyothibitishwa ya waraka katika Daftari la Ardhi ya Kijiji....................................................................... | Kanuni 54 | Kila kurasa |
17. | Ombi la nakala ya cheti ya hakimiliki ya Kimila (FAV. 22)............................................................................. | Kanuni 54 | 650/= |
18. | Usajili wa mrithi wa hakimiliki ya kimila......................... | 750/= |
|
19. | Ombi lolote kutoka kwenye Daftari la Ardhi ya Kijiji ambalo halijatajwa........................................................ | 800/= |
|
20. | Ombi la uamuzi kwa eneo maalum (FAV Na. 44)............ | 49 | 1,500/= |
21. | Msaada wa Afisa wa Masijala ya Ardhi ya Kijiji kuta-yarisha waraka wowote unaohusu shughuli, uhamishaji au jambo lolote chini ya Sheria ya Ardhi ya Vijiji............................................................................ | 1,200/= |
JEDWALI LA TATU
FAINI
(Chini ya Kifungu cha 82)
1. | Kutokutunza ardhi katika hali njema....................................... | 1,000/= |
2. | Kutolima shamba kwa utaratibu mzuri kulingana na desturi za ulimaji bora unaotumika katika eneo husika ............................ | 250/= kwa ekari |
3. | Kutumia ardhi bila kufuata utaratibu endelevu unaotunza ardhi kulingana na maadili bora na ya upeo wa juu wa ufugaji kwa mujibu wa mila na desturi katika eneo husika ......................... | 250/= |
4. | Kufanya ujenzi kabla ya kupata kibali kinachoruhusu ujenzi ..... | 750/= |
5. | Kutokulipa kodi ya pango, ada, karo, ushuru na malipo mengineyo yanayopaswa kulipwa kuhusiana na kukalia ardhi | 1% kwa mwezi |
6. | Kushindwa kulinda na kutunza salama alama za mpaka ziwe za asili au vinginevyo zilizo mipakani mwa kiwanja................................................................................ | 500/= |
7. | Kutoishi katika kijiji .............................................................. | kwa mwezi |
8. | Kuhakikisha hakimiliki ya kimila au sehemu yake kwa mtu au kikundi cha watu ambao kwa kawaida si wakazi wa kijiji bila kibali cha Halmashauri ......................................................... | 1,500/= |
9. | Kushindwa kufuta au kujihusisha na uhakilishaji wa haki miliki ya kimila ambao umekatazwa na Halmashauri ya Kijiji ............ | 2,000/= |
10. | Kutoa hakimiliki isiyo ya asili (isipokuwa kunakofanyika kwa mujibu wa Kitungu cha (4) cha Fungu la 31) bila kibali cha Halmashauri ya Kijiji ............................................................. | 1,200/= |
11. | Kurudia au ukiukaji mara kwa mara wa masharti ..................... | 2,000/= |